logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Larry Madowo apandishwa cheo CNN

Kabla ya kujiunga na CNN mwezi Mei mwaka huu Madowo alikuwa ameajiriwa kwa kampuni ingine ya kimataifa BBC kama mwandishi wa habari maeneo ya Marekani Kaskizini.

image
na Radio Jambo

Habari22 July 2021 - 03:16

Muhtasari


•Miezi miwili tu baada ya mzaliwa huyo wa Siaya, Kenya kujiunga na CNN kama mwandishi wa habari anayeripotia Nairobi, sasa amepandishwa cheo na atakuwa mwandishi wa habari wa kimataifa katika kampuni hiyo.

•Madowo alianza taaluma yake ya wandishi wa habari katika runinga ya KTN kabla ya kujiunga na NTV. Aliwahi kufanya kazi katika stesheni ya CNBC Africa nchini Afrika Kusini.

madowo1

Nyota ya mwanahabari Larry Madowo imeendelea kung'aa kila uchao huku akiendelea kupata mafanikio makubwa kwenye taaluma ya uandishi wa habari.

Miezi miwili tu baada ya mzaliwa huyo wa Siaya, Kenya kujiunga na CNN kama mwandishi wa habari anayeripotia Nairobi, sasa amepandishwa cheo na atakuwa mwandishi wa habari wa kimataifa katika kampuni hiyo.

Madowo, 34, alitangaza mafanikio hayo kupitia mtandao wa Facebook na kuweka wazi kuwa amehamia jijini Atlanta, Georgia ambako atakuwa akifanyia kazi.

Kabla ya kujiunga na CNN mwezi Mei mwaka huu Madowo alikuwa ameajiriwa kwa kampuni ingine ya kimataifa BBC kama mwandishi wa habari maeneo ya Marekani Kaskizini.

Madowo alianza taaluma yake ya wandishi wa habari katika runinga ya KTN kabla ya kujiunga na NTV. Aliwahi kufanya kazi katika stesheni ya CNBC Africa nchini Afrika Kusini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved