logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Familia yangu wameshuhudia ukarimu wako,'Msanii Akothee azidi kumlimbikizia sifa baby daddy wake

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Akothee amemlimbkizia sifa baby Daddy wake tena

image
na Radio Jambo

Habari22 July 2021 - 20:15

Muhtasari


  • Msanii Akothee azidi kumlimbikizia sifa baby daddy wake

Akothee almaarufu kama Madam Boss ni mama mwenye furaha baada ya kuwapokea wanawe wawili Prince Ojwang na Prince Oyoo nchini kutoka Ufaransa.

Wawili hao walitua katika uwanja wa ndege wa JKIA usiku wakiandamana na baba mzazi wa Oyoo ajulikanaye kama Dominic na ambaye wanaishi naye.

Akothee ambaye alikuwa ameandamana na binti wake wawili Rue Baby na Vesha Okello kuwalaki alionekana mwenye bashasha si haba kuwaona wanawe baada ya kipindi kirefu.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Akothee amemlimbkizia sifa baby Daddy wake tena huku akimshukuru kwa kukaa naye na kumuelewa.

"Nikupeleke KWA mamangu na babangu ,wakuombee mola, KWA kunitunza Mimi pamoja na wanangu🙏

👉Familia yangu , Wameshuhudia ukarimu wako wakiwa bado wako hai, sisi kama familia tunakushukuru KWA kumvumilia kichaa chetu Akothee,twajua amekukosea KWA saaaanaaaa Ila wampenda vivyo hivyo," Aliandika Akothee.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved