logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makiwa! Mume wa waziri Amina Mohamed aaga dunia baada ya kuugua kwa kipindi kifupi

Msemaji wa familia amesema kuwa msiba huo ulitokea mida ya saa kumi na moja asubuhi.

image
na Radio Jambo

Habari29 July 2021 - 06:29

Muhtasari


•Familia imesema kuwa Khalid Ahmed aliaga akiwa anapokea matibabu katika hopitali ya Karen asubuhi ya Alhamisi  baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.

•Khalid ambaye ni baba wa wawili hakuonekana sana hadharani kwani alishughulika sana na familia na uendeleshaji wa mabiashara ya familia.

Waziri wa michezo Amina Mohammed na mumewe Khalid Ahmed

Mumewe waziri wa michezo Amina Mohamed ameaga dunia.

Familia imesema kuwa Khalid Ahmed aliaga akiwa anapokea matibabu katika hopitali ya Karen asubuhi ya Alhamisi  baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.

Msemaji wa familia amesema kuwa msiba huo ulitokea mida ya saa kumi na moja asubuhi.

Khalid ambaye ni baba wa wawili hakuonekana sana hadharani kwani alishughulika sana na familia na uendeleshaji wa mabiashara ya familia.

Maafisa waku serikalini walikimbia nyumbani kwa Amina punde baada ya kupokea habari hizo huku mipango ya mazishi ikiendelea.

Familia inasema kuwa waziri Amina ameathirika zaidi kuona kuwa miezi minne iliyopita alipoteza ndugu yake Esmael Mohammed Jibril ambaye alikuwa mwanabiashara ashuhuri nchini.

Jibril aliaga mwezi Machi alipokuwa anapokea matibabu nchini India.

Mengine mengi yatafuata....

 

(Utafsiri; Samuel Maina)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved