logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Hafla ya mazishi ya afisa Caroline Kangogo aliyeripotiwa kujitoa uhai yaendelea

Mwili wa Caroline ulivalishwa gauni la harusi kama alivyokuwa ameomba kupitia ujumbe wa simu.

image
na Radio Jambo

Habari29 July 2021 - 07:58

Muhtasari


•Hafla ya mazishi  ya afisa Caroline Kangogo aliyeripotiwa kujiotoa uhai mnamo Julai  16 iling'oa nanga asubuhi ya Alamisi.

•Mamia ya waombolezaji ikiwemo maafisa wa polisi kutoka kituo cha polisi cha Nakuru alikokuwa anahudumu Bi Caroline walihudhuria. 

Jeneza la marehemu Caroline Kangogo

Hafla ya mazishi  ya afisa Caroline Kangogo aliyeripotiwa kujiotoa uhai mnamo Julai  16 iling'oa nanga asubuhi ya Alamisi.

Mwili wa marehemu ulisafirishwa kwa gari la kubebea maiti na maafisa wa polisi hawakuhusishwa kwenye shughuli hiyo.

Wazazi wa Caroline, Bw Barnabas Kangogo na Bi Leah Kangogo waliongoza waombolezaji kuchukua mwili wa  marehemu kutoka chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Iten.

Wazazi wa marehemu Caroline Kangogo, Bwana Barnabas Kangogo na Bi Leah Kangogo

Mwili wa Caroline ulivalishwa gauni la harusi kama alivyokuwa ameomba kupitia ujumbe wa simu.

Kakake marehemu, Mark Kangogo alisema kuwa dadake  alikuwa mtu mzuri licha ya yale yaliandikwa kumhusu kwenye vyombo vya habari. Alisema kuwa familia itamfanyia marehemu mazishi ya heshima.

Mamia ya waombolezaji ikiwemo maafisa wa polisi kutoka kituo cha polisi cha Nakuru alikokuwa anahudumu Bi Caroline walihudhuria. 

Aliyekuwa bwana wa Caroline, Bw. Ngeno pia alihudhuria hafla hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved