logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal yanasa saini ya mlinzi Ben White kwa pauni 50M

Mlinzi wa timu ya kitaifa ya Uingereza Ben White atavalia jazi nyekundu msimu ujao baada ya kukamilisha uhamisho wa kujiunga na klabu ya Arsenal kutoka Brighton & Hoves Albion.

image
na Radio Jambo

Habari31 July 2021 - 04:40

Muhtasari


•Arsenal iltoa tangazo rasmi kuhusu uhamisho huo siku ya Alhamisi baada ya mchezaji huyo kutia saini mkataba wa miaka mitano.

•White alihusishwa katika kikosi cha Uingereza ambacho kilicheza katika michuano ya Euro 2020 na kumaliza wa pili baada ya kupigwa na Italia kwenye fainali.

Kocha Mikel Arteta, Ben White na Edu

Mlinzi wa timu ya kitaifa ya Uingereza Ben White atavalia jazi nyekundu msimu ujao baada ya kukamilisha uhamisho wa kujiunga na klabu ya Arsenal kutoka Brighton & Hoves Albion.

Arsenal iltoa tangazo rasmi kuhusu uhamisho huo siku ya Alhamisi baada ya mchezaji huyo kutia saini mkataba wa miaka mitano.

"Ben White amejiunga nasi kutoka Brighton  & Hove Albion kwa kandarasi ya miaka mingi. Mlinzi huyo wa miaka 23 ambaye amejionyesha kuwa mmoja wa wachezaji wadogo wazuri anajiunga nasi baada ya kuhusishwa kwenye kikosi cha Uingereza kilichocheza kwenye Euro" Arsenal ilitangaza kupitia tovuti yake rasmi.

Inafahamika kuwa White, 23, aligharimu Arsenal pauni milioni 50 na atavalia jazi nambari 4.

White alihusishwa katika kikosi cha Uingereza ambacho kilicheza katika michuano ya Euro 2020 na kumaliza wa pili baada ya kupigwa na Italia kwenye fainali.

Arsenal imekuwa ikiwinda mchezaji huyo matata mwenye umri wa ujana kwa muda sasa.

White alisema kuwa alifurahia sana kujiunga na klabu hiyo ya London.

"Imechukua muda kuliko nilivyotarajia ila nafurahia kuwa hapa sasa" White alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved