logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gor Mahia yatangaza usajili wa kocha mpya

Kocha Harrison ambaye ana umri wa miaka 60 aliwahi chezea klabu tajika Uingereza kama Southampton, Stoke City na Port Vale.

image
na Radio Jambo

Habari03 August 2021 - 07:19

Muhtasari


•Klabu ya Gor Mahia imetangaza kocha wake mpya wiki tatu tu baada ya kujiuzulu kwa aliyeshikilia wadhfa huyo Manuel Pinto kutoka Ureno.

•Siku za uchezaji wake, Harrison alicheza katika nafasi ya mlinda lango.

Kocha Mark Harrison azinduliwa

Klabu ya Gor Mahia imetangaza kocha wake mpya wiki tatu tu baada ya kujiuzulu kwa aliyeshikilia wadhfa huyo Manuel Pinto kutoka Ureno.

K'Ogallo ilitangaza uteuzi wa Mark Harrison kutoka Uingereza  kama kocha mpya Jumatatu jioni.

Meneja huyo mzaliwa wa Uingereza atakuwa na jukumu kubwa kujaribu kurejesha ubora wa mabingwa hao msimu uliopitia ambao hivi karibuni wamekuwa wakiandikisha matokeo hafifu.

Kocha Harrison ambaye ana umri wa miaka 60 aliwahi chezea klabu tajika Uingereza kama Southampton, Stoke City na Port Vale.

Siku za uchezaji wake, Harrison alicheza katika nafasi ya mlinda lango. Amekuwa kwenye taaluma ya kufunza na kusimamia klabu za kandanda kwa miaka zaidi  20.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved