logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri wa Ulinzi nchini Tanzania afariki dunia

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini humo, Jenerali Venance Mabeyo

image
na Radio Jambo

Habari03 August 2021 - 05:21

Muhtasari


•Waziri Kwandikwa, alikuwa akipata matibabu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa karibu siku kumi na nne.

•Rais Samia amesema amepokea kwa masikitiko kifo cha waziri huyo kutokana na mchango wake mkubwa katika utumishi wa Umma.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa nchini Tanzania, Elias Kwandikwa, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam.

Waziri Kwandikwa, alikuwa akipata matibabu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa karibu siku kumi na nne.

Kwandikwa pia ni mbunge wa Ushetu katika mkoa wa Shinyanga.

Katibu wa Mbunge huyo, Julius Lugobi amethibitishia Mwananchi Digital kuwa Mbunge huyo ameaga dunia hapo jana.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini humo, Jenerali Venance Mabeyo, Taarifa kutoka Ikulu imeeleza.

Rais Samia amesema amepokea kwa masikitiko kifo cha waziri huyo kutokana na mchango wake mkubwa katika utumishi wa Umma.

‘’Tumepoteza mtu muhimu ambaye mchango wake katika utumishi wa Umma hautasahaulika, Kwandikwa alikuwa kiongozi shupavu ambaye alikuwa akitekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria na taratibu’’. Alisema Rais Samia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved