logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wengine walitupatia miezi miwili" Vera Sidika awasuta waliodai kuwa ndoa yake na Mauzo haingedumu

Mama huyo mtarajiwa amesema kuwa kunao ambao walidai kuwa uhusiano wao haungedumu kwa zaidi ya miezi miwili huku wengine walisema kuwa yeye huwa na na mume tofauti kila anapoadhimisha siku ya kuzaliwa.

image
na Radio Jambo

Mahakama15 August 2021 - 13:02

Muhtasari


•Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera amesema kuwa walichumbiana kisiri na mpenziwe kwa kipindi cha miezi miwili kabla ya kuweka uhusiano wao hadharani.

•Kulingana na mwanasoshalaiti huyo mwenye umri wa miaka 31, kunao watu wengi ambao hawapendi kuona wengine wakifanikiwa kimahusiano, kibiashahara na kwa mambo mengine maishani.

•Wawili hao walijitosa kwenye ndoa mnamo Agosti 12 mwaka uliopita na mapenzi yao yameendelea kunoga huku sasa wakiwa safarini kuanzisha familia ndogo.

Mwanasoshalaiti na mjasiriamali mashuhuri Veronica Mung'asia almaarufu kama Vera Sidika amewasuta wale ambao hawakuamini kuwa ndoa yake na mwanamuziki Brown Mauzo ingedumu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera amesema kuwa walichumbiana kisiri na mpenziwe kwa kipindi cha miezi miwili kabla ya kuweka uhusiano wao hadharani.

Amesema kuwa walipojitokeza wengi hawakuamini kuwa ni kweli walikuwa wamefunga ndoa huku baadhi ya wanamitandao kwa wakati ule wakidai kuwa ilikuwa kiki.

"Nakumbuka tukianza kuchumbiana tulikuwa tumejificha kisha tukatangaza hadharani miezi miwili baadae. Kila mtu alidai kuwa ni kiki" Vera alisema.

Mama huyo mtarajiwa amesema kuwa kunao ambao walidai kuwa uhusiano wao haungedumu kwa zaidi ya miezi miwili huku wengine walisema kuwa yeye huwa na na mume tofauti kila anapoadhimisha siku ya kuzaliwa.

"Wengine walisema kuwa kila ninapoadhimisha siku ya kuzaliwa mimi huwa na mwanaume tofauti. Basi ninasherehekea siku ya kuzaliwa hivi karibuni. Wengine walitupatia miezi miwili na baada ya miezi miwili kuisha wakaongeza miezi mitatu. Ilifika hatua wakapoteza matumaini" Aliendelea kusema.

Kulingana na mwanasoshalaiti huyo mwenye umri wa miaka 31, kunao watu wengi ambao hawapendi kuona wengine wakifanikiwa kimahusiano, kibiashahara na kwa mambo mengine maishani.

" Mimi husema, amini Mungu na kila kitu kitakuwa sawa kila wakati. Mungu anajua kuaibisha adui zako" Vera alisema.

Siku ya Alhamisi, Agosti 12 Vera na kipenzi chake Brown Mauzo waliadhimisha mwaka mmoja wa ndoa yao.

Wawili hao walijitosa kwenye ndoa mnamo Agosti 12 mwaka uliopita na mapenzi yao yameendelea kunoga huku sasa wakiwa safarini kuanzisha familia ndogo.

Siku chache zilizopita mwanasoshalaiti huyo alishangaza wanamitandao baada ya kukiri kuwa uhusiano wake wa sasa na mwanamuziki Brown Mauzo ndio mrefu zaidi kuwahi tokea maishani mwake. 

Vera Sidika alifichua kuwa kamwe hajawahi kuchumbia mwanaume mmoja kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja hapo awali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved