logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kesi ya R. Kelly: Mwathiriwa wa kiume atoa ushahidi wa unyanyasaji wa kingono

Mwanamume huyo aliyetoa Ushahidi kwa kutumia jina la kisiri la Louis, alisema alikuwa na miaka 17 wakati Bwana Kelly alipomuuliza "yuko tayari kufanya nini kwa ajili ya muziki".

image
na Radio Jambo

Habari31 August 2021 - 15:38

Muhtasari


•.Mwanamume huyo aliyetoa Ushahidi kwa kutumia jina la kisiri la Louis, alisema alikuwa na miaka 17 wakati Bwana Kelly alipomuuliza "yuko tayari kufanya nini kwa ajili ya muziki".

•Aliiambia mahakama kuwa Bw. Kelly alimpatia namba ya simu na kumkaribisha nyumbani kwake, akisema angeweza kutumbuiza katika studio ya kurekodi na kupokea vidokezo kadhaa kwenye biasharaya muziki.

Kesi ya msanii R. Kelly kuhusu unyanyasaji wa kingono imeingi asiku ya nane Jumatatu , huku mlalamishi wa kiume akitoa Ushahidi kwamba nyota huyo wa muziki alimuahidi umaarufu akikubali kufanya ngono naye.

Mwanamume huyo aliyetoa Ushahidi kwa kutumia jina la kisiri la Louis, alisema alikuwa na miaka 17 wakati Bwana Kelly alipomuuliza "yuko tayari kufanya nini kwa ajili ya muziki".

Kisha akelezea jinsi mwanamuziki huyo alivyotambaakuelekea kwake akifanya onyesho la kimapenzi , ijapokuwa "sikutaka kujihusisha na hayo".

Bwana Kelly, 54, amekanusha mashtaka yote dhidi yake.

Hii ni pamoja na hshtaka moja la udanganyifu - ambayo inamuonyesha kama mkuu wa biashara ya jinai ambayo lengo lake lilikuwa "kuwateka wanawake wadogo na vijana" kwa madhumuni ya ngono - na makosa manane ya kukiuka sheria ya biashara ya ngono inayojulikana kama Sheria ya Mann.

Mwimbaji huyo ambaye jina lake kamili ni Robert Kelly, hajashtakiwa kwa ubakaji na kushambulia, lakini waendesha mashtaka wanaruhusiwa kutoa ushahidi wa uhalifu wowote unaohusiana na mashtaka ya ujambazi, bila kujali ni lini ulitokea.

Aliiambia mahakama kuwa Bw. Kelly alimpatia namba ya simu na kumkaribisha nyumbani kwake, akisema angeweza kutumbuiza katika studio ya kurekodi na kupokea vidokezo kadhaa kwenye biasharaya muziki.

Siku ya Jumatatu, majaji walisikia ushahidi wa waathiriwa wawili, wote wanasema walikuwa watoto wakati walipokutana na na Bw.Kelly.

Louis alisema alikutana mara ya kwanza na Bw. Kelly mwaka 2006, akiwa na miaka 17-akifanya kazi nyakati za usiku katika McDonald's mjini Chicago.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved