logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+PICHA)Mwandishi wa habari wa gazetti la the Star Corazon Wafula azikwa Turbo

Alikufa akiwa na umri wa miaka 32 na ameacha mtoto mmoja.

image
na Radio Jambo

Habari04 September 2021 - 13:54

Muhtasari


  • Mwanahabari wa gazetti la the Star Corazon Kwamboka azikwa Turbo

Mwandishi wa gazetti la the Star Corazon Wafula amelazwa, nyumbani kwao Turbo.

Sherehe ya mazishi ya Corazon ilifanyika Jumamosi nyumbani kwake kwa familia huko Turbo, Eldoret.

Corazon au Cora kama baadhi ya marafiki wake walikuwa wakimuita aliaga dunia baada ya kuugua ugonjwa wa ini ugonjwa wa tezi, hali ambayo alikuwa akipambana nayo kwa muda mrefu.

Alikufa akiwa na umri wa miaka 32 na ameacha mtoto mmoja.

Huku pacha wake akizungumzia jinsi walikuwa wanaishi, na jinsi alikuwa anapenda kazi yake alikuwa na haya ya kusema.

"Kila wakati tuliposafiri, Cora kila wakati alikuwa akiwasha kompyuta yake ndogo. Tungemwambia 'weka mbali kompyuta na tusimulie hadithi lakini angesema' kuna hadithi hii ninayoifuata, sitaki inipite, "Winnie, dada yake pacha, alisema.

Mungu azidi kuilaza roho yake mahali pema peponi.

Hizi hapa baadhi ya picha za hafla hiyo;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved