logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwigizaji mashuhuri wa filamu 'The Wire' apatikana amefariki ndani ya nyumba yake

Williams 54, ambaye alicheza kama 'Omar Little' kwenye filamu ya 'The Wire' alipatikana akiwa ameaga ndani ya nyumba yake jijini New York siku ya Jumatatu

image
na Radio Jambo

Habari07 September 2021 - 10:04

Muhtasari


•Inatuhumiwa kuwa mwigizaji huyo aliangamia kutokana na utumiaji wa madawa ya kulevya kupita kiasi, ingawa madai hayo hayajathibitishwa bado.

Mwigizaji wa Marekani Michael K Williams  anayefahamika sana kutokana na filamu 'The Wire' ameaga dunia.

Williams 54, ambaye alicheza kama 'Omar Little' kwenye filamu ya 'The Wire' alipatikana akiwa ameaga ndani ya nyumba yake jijini New York siku ya Jumatatu . Aliigiza kama shoga, jambazi na muuzaji wa madawa ya kulevya.

Inatuhumiwa kuwa mwigizaji huyo aliangamia kutokana na utumiaji wa madawa ya kulevya kupita kiasi, ingawa madai hayo hayajathibitishwa bado.

Mwili wa Williams ulipatikana katika chumba chake cha maakuli huku kichwa chake kikiwa kimetazama chini. Inaripotiwa kuwa poda iliyoonekana kuwa heroin ilipatikana juu ya meza yake.

Baadhi ya waiigizaji wenzake na watengeneza filamu wametuma risala za rambirambi.

Hapo awali, Williams ambaye alikuwa ameteuliwa mara tatu kupokea tuzo la Emmy alikuwa amefunguka kuhusu shida yake ya utumizi wa madawa ya kulevya kwa miaka mingi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved