logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona: Watu 661 wapatikana na corona,533 wapona ,32 waaga dunia

Mgonjwa wa umri wa chini ana siku 11, huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 102.

image
na Radio Jambo

Habari10 September 2021 - 14:19

Muhtasari


  • Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 640 ni wakenya ilhali 21 ni raia wa kigeni,332 ni wanaume huku 329 wakiwa wanawake
  • Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 2412,945 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 8.1%
Waziri Mutahi Kagwe

Watu 661 wamepatikana na maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 8,141 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 640 ni wakenya ilhali 21 ni raia wa kigeni,332 ni wanaume huku 329 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 2412,945 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 8.1%.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,444,357.

Mgonjwa wa umri wa chini ana siku 11, huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 102.

Hata hivyo watu 32 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 4,896 ya walioaga dunia.

Aidha watu 533 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 230,940, 416 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 117 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Kuna wagonjwa 1,723 ambao wamelazwa hospitalini, 4,725 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 174  katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved