logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Siwezi enda mahojiano kuulizwa juu ya ndugu yangu,'Bahati afunguka kuhusu uhusiano wake na Mr Seed

Pia alimsifia na kusema kwamba ni mama bora zaidi duniani.

image
na Radio Jambo

Habari13 September 2021 - 09:34

Muhtasari


  • Msanii Bahati kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu uhusiano wake na msanii Mr Seed baada ya wawili hao kukosana miaka chache iliyopita

Msanii Bahati kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu uhusiano wake na msanii Mr Seed baada ya wawili hao kukosana miaka chache iliyopita.

KUlingana na Bahati  uhusiano wake na Mr Seed hauwezi isha kwa ajili ya mambo ambayo yaliandikwa wala kusemwa kwenye mitandao ya kijamii.

"Niliacha kuenda kwenye mahojiano, baada ya wanablogu kueneza maneno mengi kati yangu na Mr Seed, siwezi enda mahojiano kuulizwa kuhusu ndugu yangu Seed

Lica ya yote ambayo tumefanyiana na Seed hayawezi funika kumbukumbu ambazo nimekuwa nazo nikiwa na Seed," Alisema Bahati.

Pia msanii huyo alifichua kwamba licha ya yote ambayo yalisemwa alikuwa anamtembelea mama Seed, na hajawahi muuliza chochote.

Pia alimsifia na kusema kwamba ni mama bora zaidi duniani.

"Baada ya mambo mengi kuandikwa, nilikuwa namtembelea mama Seed, na ahajawahi niuliza chochote kuhusu uhusiano wangu na Seed

Ni mama bora zaidi ambaye nimewahi kutana naye."

Pia aliwatania Mr Seed na mkewe kwa kuwaambia kwamba wanapaswa kuongeza mtoto mwingine.

"Nimo nataka muoongee mtoto mwingine nangoja, Mr Seed nakupenda sana na nakutakia kila laheri katika albamu yako mpya."

Bahati alizungumza hayo wakati wa uzinduzi wa albamu mpya ya Mr Seed, halfala ambayo ilihudhuriwa na familia, marafiki,wasanii wenzake miongoni mwa watu wengine.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved