logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko Homabay baada ya mwanajeshi wa zamani kuua mamake kwa kisu kufuatia mgogoro wa shamba

Inadaiwa kwamba wawili hao walizozana kwa kipindi kifupi kisha jamaa huyo kuchukua kisu na kumdunga mama yake kifuani na kwenye kichwa.

image
na Radio Jambo

Habari14 September 2021 - 02:50

Muhtasari


•Richard Odak ambaye alikuwa mwanajeshi nchini Tanzania anadaiwa kuua mamake Hellen Ajwang Odiango 91, nyumbani kwao katika eneo la Kamagak Magharibi, kaunti ndogo ya Kasipul

•Kufuatia  mgogoro huo Odak anaripotiwa kuondoka nyumbani kwao mwaka uliopita na kuenda mahali kusikojulikana kisha kurejea siku ya Ijumaa wiki iliyopita na kuanza kogombana na mamaye kama ilivyokuwa kawaida

Crime scene

Habari na Robert Omollo

Polisi katika kaunti ya Homabay wanasaka jamaa mmoja ambaye ni mwanajeshi wa zamani anayetuhumiwa kuua mamaye kufuatia mzozo wa shamba.

Richard Odak ambaye alikuwa mwanajeshi nchini Tanzania anadaiwa kuua mamake Hellen Ajwang Odiango 91, nyumbani kwao katika eneo la Kamagak Magharibi, kaunti ndogo ya Kasipul.

Inasemekana kuwa mshukiwa amekuwa akizozana na mamake kuhusu shamba hilo kwa kipindi kirefu. Odak amejenga nyumba yake pale.

Kufuatia  mgogoro huo Odak anaripotiwa kuondoka nyumbani kwao mwaka uliopita na kuenda mahali kusikojulikana kisha kurejea siku ya Ijumaa wiki iliyopita na kuanza kogombana na mamaye kama ilivyokuwa kawaida.

Inadaiwa kwamba wawili hao walizozana kwa kipindi kifupi kisha jamaa huyo kuchukua kisu na kumdunga mama yake kifuani na kwenye kichwa.

Baada ya hayo Bi Odiango alikimbizwa katika hospitali ya Rachuonyo Kusini ambako alifariki kutokana na majeraha mabaya ambayo alikuwa amepata mwilini.

Kamanda wa polisi katika eneo la Rachuonyo Kusini Lilies Wachira alisema kuwa mshukiwa alitoweka punde baada ya kutekeleza mauaji yale.

Uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo umeng'oa nanga huku juhudi za kumsaka mshukiwa ambaye alikuwa akiishi Tanzania zikiendelea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved