logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona:Kenya imesajili visa 446 vipya vya maambukizi ya corona

Mgonjwa wa umri wa chini ana wiki 2 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 101.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2021 - 13:56

Muhtasari


  • Watu 446 wamepatikana na maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 6,406 chini ya saa 24 zilizopita
  • Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 435 ni wakenya ilhali 11 ni raia wa kigeni,227 ni wanaume huku 2019 wakiwa wanawake
MAJARIBIO YA CHANJO: Chanjo mpya ya Pfizer na BioNTech ina kinga ya asilimia 90 Picha: REUTERS

Watu 446 wamepatikana na maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 6,406 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 435 ni wakenya ilhali 11 ni raia wa kigeni,227 ni wanaume huku 2019 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 244,826 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 7.0%.

Mgonjwa wa umri wa chini ana wiki 2 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 101.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,470,865.

Hata hivyo watu 21 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 4,949 ya walioaga dunia.

Aidha watu 459 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 235,196, 331 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 128 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Kuna wagonjwa 1,525 ambao wamelazwa hospitalini, 3,341 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 118  katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved