logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu wengi wameenda shule lakini elimu haijawasaidia-Nyota awasuta wenye tabia ya kuwakejeli watu mitandaoni

Nyota amewaambia wenye tabia hiyo, baada ya kutoa maoni ya kukejeli mtu wanapaswa kufikiria.

image
na Radio Jambo

Habari19 September 2021 - 08:38

Muhtasari


  • Nyota awasuta wenye tabia ya kuwakejeli watu mitandaoni

Msanii kutoka mkoa wa wapi Nyota Ndogo kwa mara nyingine amewaka moto mitandaoni baada ya kuwasuta wanamitandao ambao wanatabia ya kukejeli watu wanapopakia chochote kwenye kurasa zao za mitandao.

KUpitia kwenye ukurasa wake wa instagram msanii huyo amepakia video , na kusema kwamba anaelewa watu wameenda shule lakini kuna wale elimu yao haijawasaidia.

Nyota amewaambia wenye tabia hiyo, baada ya kutoa maoni ya kukejeli mtu wanapaswa kufikiria.

"Kitu ambacho nimegundua watu kwenye mitandao ya kijamii, unapopakia kitu kwenye ukurasa wako mwenye, nimekuja kugundua watu wameenda shule lakini elimu haijawasaidia

Usikimbilie kutoa maoni yako,kwanza soma na uhakikishe kwamba umeelewa nini haswa kimepakiwa pale

Lakini kwa sababu wana vidole na simu, wanatoa maoni kwa jambo ambalo hawajaelewa umemaanisha nini

Tafadhali kabla hujatoa maoni yako kuhusu chochote elewa," Alisema Nyota.

Pia alizidi na kusema

"Kila siku tunaambiwa hatujasoma na wengi waliosoma hali yetu, watu na viatu."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved