logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nilikuwa mwaminifu kwake sijawahi mcheza,'Fayvanny azungumzia uhusiano wake na Rayvanny

Fayvanny alifutilia mbali madai kwamba alimdanganya msanii huyo

image
na Radio Jambo

Habari01 October 2021 - 09:14

Muhtasari


  • Fayvanny azungumzia uhusiano wake na Rayvanny
fayvanny

Baby mama wa mstaa wa bongo Rayvanny, Fayvanny kwa mara ya kwanza amezungumzia nini haswa kilifanya watengane na msanii huyo.

Fayvanny alifutilia mbali madai kwamba alimdanganya msanii huyo na kuongeza kwamba alikuwa mwaminifu kwake.

Akiwa kwenye mahojiano, Fayvanny alisema kwamba alishangaa sana baada ya madai kwamba ni yeye alimdanganya msanii huyo.

"Hapana nimekataa, sijawahi mdanganya au mcheza,mtafuteni Rayvanny na mumuulize, wwacha nimseme nilikuwa mwaminifu kwake na sijawahi mcheza

Nimeshangaa sana kuwa watu wanaweza sema jambo hilo au madai kama hayo juu yangu," Aliongea Fayvanny.

Pia alisema kwamba ni mapenzi ya Mungu waliachana, hii ni baada ya kuulizwa sababu ya kutengana na baba wa mtoto wake.

"Ni mapenzi yake Mungu."

Wawili hao wamebarikiwa na mtoto mmoja, lakini Rayvanny amethibitisha kwamba ameshaaendelea na maisha yake baada ya kuachana na mama wa mtoto wake.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved