logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mke wangu ndiye Mali ya bei ghali zaidi ninayomiliki hivi sasa,'Jimal Roho Safi afichua

Baada ya uhusiano wake na Amber Ray kuisha, Jimal alimrudia mke wake wa kwanza

image
na Radio Jambo

Habari18 October 2021 - 19:41

Muhtasari


  • Mfanyibiashara Jimal Roho Safi alifahamika sana baada a kumuoa mwanasosholaiti Amber Ray mapema mwaka huu

Mfanyibiashara Jimal Roho Safi alifahamika sana baada a kumuoa mwanasosholaiti Amber Ray mapema mwaka huu.

Uhusiano wao ulikuwa na vizuizi vingi kwani alikuwa na mke wa kwanza,ambaye wamebarikiwa naye watoto wawili.

Akiwa kwenye mahojiano na Radiojambo Amira alisema kwamba alifahamu uhusiano wa mumewe na Amber kupitia kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya uhusiano wake na Amber Ray kuisha, Jimal alimrudia mke wake wa kwanza na ambaye amekuwa akimridhisha kwa kila jambo ili kumuomba msamaha kwa yale yalitokea.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram , Jimal alijibu swali ambalo aliulizwa nini haswa kitu cha bei ghali anachomiliki kwa sasa.

Kulingana na Jimal Mali ya bei ghali zaidi ninayomiliki hivi sasa ni mke wake;

"Ni mali ipi ghali zaidi unayomiliki sasa?"

Mimi Mke wangu,"Jimal alijibu.

Tunatumai ndoa yake Jimal na mkewe itaendelea, na mapenzi yao yataendelea kunoga kila kuchao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved