logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Walimu 2 wanaodaiwa kutoroka na pesa walizopatiwa na mwanasiasa wagawe wanusuriwa kwa umati uliotaka kuwaadhibu, Makueni

Iliripotiwa kuwa walimu hao walipopokea pesa zile walikosa kugawia waendesha bodaboda wale pamoja na wanawake waliokuwa wanauza bidhaa sokoni na wakaamua kutoroka nazo zote.

image
na Radio Jambo

Habari26 October 2021 - 08:53

Muhtasari


•Wawili hao ambao ni walimu katika shule ya msingi walikimbia katika kituo cha polisi cha Kambu na kujificha nyuma ya meza ya kupigia ripoti huku kikundi kikubwa cha waendesha bodaboda kikiwa kimewaandama unyo kwa unyo.

•Iliripotiwa kuwa walimu hao walipopokea pesa zile walikosa kugawia waendesha bodaboda wale pamoja na wanawake waliokuwa wanauza bidhaa sokoni na wakaamua kutoroka nazo zote.

crime scene

Walimu wawili katika kaunti ya Makueni wanaodaiwa kupokea kitita cha shilingi milioni moja kutoka kwa mwanasiasa aliyekuwa amezuru eneo hilo walinusurika kifo baada ya polisi kuwaokoa kutoka kwa kikundi cha waendesha bodaboda waliotaka kuwaangamiza.  

Kulingana na Dci, wawili hao ambao ni walimu katika shule ya msingi walikimbia katika kituo cha polisi cha Kambu na kujificha nyuma ya meza ya kupigia ripoti huku kikundi kikubwa cha waendesha bodaboda kikiwa kimewaandama unyo kwa unyo.

Polisi wawili waliokuwa kituoni walipata wakati mgumu kujaribu kuthibiti waendesha bodaboda hao ambao walitaka kupata sehemu ya pesa ambazo walidai walimu wale walikuwa wamepokea. 

Iliripotiwa kuwa walimu hao walipopokea pesa zile walikosa kugawia waendesha bodaboda wale pamoja na wanawake waliokuwa wanauza bidhaa sokoni na wakaamua kutoroka nazo zote.

Kufuatia madai hayo waendesha bodaboda wale walianza kuwakimbiza walimu hao wakidai kuwaangamiza kutokana na kile walisema ni kunyang'anywa haki yao.

Waendesha bodaboda wale walianza kutupa vitu mbalimbali kituoni katika jitihada za kuwatoa walimu hao na hapo ikabidi maafisa wa polisi waliokuwepo waombe usaidizi kutoka kwa wenzao katika kituo cha Mtito Andei.

Baada ya idadi ya polisi kuongezeka kikundi kile kiliweza kutawanywa huku uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo uking'oa nanga.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved