logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Shujaa 7s, Kenya Lionesses waibuka bingwa katika mashindano ya Safari 7s

Shujaa 7s walipiga Ujerumani 12-5 katika fainali ya kukata na shoka ambayo ilifanyika siku ya Jumapili na kuwezesha Kenya kuhifadhi taji hilo ambalo lilishindwa na Kenya Morans mwaka wa 2019.

image
na Radio Jambo

Habari01 November 2021 - 03:00

Muhtasari


•Shujaa 7s walipiga Ujerumani 12-5 katika fainali ya kukata na shoka ambayo ilifanyika siku ya Jumapili na kuwezesha Kenya kuhifadhi taji hilo ambalo lilishindwa na Kenya Morans mwaka wa 2019.

•Lionesses walipata ushindi mkubwa wa 26-0 dhidi ya Uganda cranes katika fainali  ya mashindano hayo.

Timu ya taifa ya rafa Shujaa 7s iliweza kushinda mashindano ya Safari 7s 2021 ambayo yakifanyika ugani Nyayo wikendi iliyotamatika.

Shujaa 7s walipiga Ujerumani 12-5 katika fainali ya kukata na shoka ambayo ilifanyika siku ya Jumapili na kuwezesha Kenya kuhifadhi taji hilo ambalo lilishindwa na Kenya Morans mwaka wa 2019.

Alvin 'Buffa' Otieno na Johhnstone Olindi walifungia Shujaa 7s huku Jack Hunt akifungia Ujerumani.

Collins Shikoli alionyeshwa kadi nyekundu kwa kucheza katika kipindi cha pili ila jambo hilo halikukatiza matumaini ya Shujaa ya kupata ushindi. Ujerumani pia walipunguzwa hadi wachezaji sita baada ya mmoja wao kuonyeshwa kadi nyekundu muda mfupi baadae.

Timu ya wanawake ya Kenya Lionesses pia  ilibuka bingwa baada ya kushinda mechi zake zote.

Lionesses walipata ushindi mkubwa wa 26-0 dhidi ya Uganda cranes katika fainali  ya mashindano hayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved