logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Ajuza wa miaka 80 ataka kuwania kiti cha mwakilishi wa wanawake Nairobi kwa tikiti ya UDA

Bi Cecilia Mwangi almaarufu kama Shosh ambaye anamiliki duka la kuuza ala za sauti jijini Nairobi alipatana na katibu mkuu wa chama cha UDA, Veronica Maina siku ya Jumanne na kutangaza azma yake ya kuwania kiti cha mwakilishi wa wanawake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 November 2021 - 03:08

Muhtasari


•Bi Cecilia Mwangi almaarufu kama Shosh ambaye anamiliki duka la kuuza ala za sauti jijini Nairobi alipatana na katibu mkuu wa chama cha UDA, Veronica Maina siku ya Jumanne na kutangaza azma yake ya kuwania kiti cha mwakilishi wa wanawake.

Bi Cecilia Mwangi katika ofisi za UDA siku ya Jumanne

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 80 anatazamia kumbandua Esther Passaris kutoka kwa kiti chake cha mwakilishi wa wanawake katika kaunti ya Nairobi.

Bi Cecilia Mwangi almaarufu kama Shosh ambaye anamiliki duka la kuuza ala za sauti jijini Nairobi alipatana na katibu mkuu wa chama cha UDA, Veronica Maina siku ya Jumanne na kutangaza azma yake ya kuwania kiti cha mwakilishi wa wanawake.

Kupitia mtandao wa Facebook, chama cha UDA kinachohusishwa na naibu rais William Ruto kilitangaza kuwa Bi. Cecilia amejiunga rasmi na chama hicho na atakuwa katika kinyang'anyiro cha mwaka ujao.

"Cecilia Mwangi (Shosh)  80, ambaye ni mmiliki wa Shosh Sound Systems, ambaye alivuma kwenye vyombo vya habari vya kimataifa amekaribishwa UDA na katibu mkuu Generali Veronica Maina. Atawania kiti cha mwakilishi wa wanawake katika kaunti ya Nairobi" UDA ilitangaza.

Mwanasiasa mwingine ambaye anamezea mate kiti hicho na tikiti ya UDA ni seneta wa kuteuliwa Millicent Omanga.

Omanga tayari ameanza kujipigia debe na kuboresha nafasi yake ya kumbandua Passaris wa chama cha ODM ambaye alinyakua kiti hicho mwaka wa 2017.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved