logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majonzi baada ya wanafunzi 4 wa chuo kikuu cha Tharaka waliokuwa wameenda kupiga picha mtoni kufa maji

Msemaji wa polisi  Bruno Shioso alisema kundi la wanafunzi wa mwaka wa kwanza walikuwa wamekwenda mtoni kwa ajili ya kupiga picha ambapo baadhi yao waliamua kuogelea bila kujali hatari iliyowatazamia macho.

image
na Radio Jambo

Habari07 November 2021 - 06:49

Muhtasari


•Mashahidi walisimulia kwamba yote yalianza wakati mmoja wao alianza kuzama na wengine walipojaribu kumuoka wakazama pia na kufa maji.

•Msemaji wa polisi  Bruno Shioso alisema kundi la wanafunzi wa mwaka wa kwanza walikuwa wamekwenda mtoni kwa ajili ya kupiga picha ambapo baadhi yao waliamua kuogelea bila kujali hatari iliyowatazamia macho.

Habari na Cyrus Ombati

Kipindi cha kupiga picha kiligeuka kuwa msiba baada ya wanafunzi wanne kutoka Chuo Kikuu cha Tharaka kufa maji walipokuwa wanaogelea katika mto Kathita alasiri ya Jumamosi.

Kufikia usiku wa Jumamosi, miili mitatu ilikuwa imetolewa majini tayari huku msako wa mwili wa nne ukiendelea.

Msemaji wa polisi Bruno Shioso alisema kuwa miili iliyopatikana ni ya wanaume wawili na  mwanamke mmoja huku akitaja tukio hilo kuwa msiba.

Alisema kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza walikuwa wanaogelea wakati wanne kati yao walikufa maji.

Mashahidi walisimulia kwamba yote yalianza wakati mmoja wao alianza kuzama na wengine walipojaribu kumuoka wakazama pia na kufa maji.

Wanafunzi wengine wawili waliweza kunusurika baada ya wakazi kuwaokoa na kuwakimbiza hospitalini.

Kwa bahati mbaya wenzao wanne waliwezwa na mikondo ya maji yenye nguvu na kupoteza maisha yao. Miili iliyopatikana ilipelekwa katika mochari ya Marimanti.

Shioso alisema kundi la wanafunzi wa mwaka wa kwanza walikuwa wamekwenda mtoni kwa ajili ya kupiga picha ambapo baadhi yao waliamua kuogelea bila kujali hatari iliyowatazamia macho.

Alisema kuwa wazazi wa wahasiriwa tayari walikuwa wamefahamishwa kuhusu tukio hilo la kuhofisha,

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved