logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shughuli zote za ligi za FKF nchini zimesimamishwa

Uahirisho ambao utaanza kutumika mara moja utaendelea kwa muda wa wiki mbili, kuanzia leo.

image
na Radio Jambo

Habari12 November 2021 - 12:08

Muhtasari


  • Kamati mpya ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) imesimamisha shughuli zote za kandanda kote nchini mara moja

Kamati mpya ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) imesimamisha shughuli zote za kandanda kote nchini mara moja.

 Aaron Ringera aliyeongoza kamati ya muda, kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, iliyotolewa Ijumaa, Novemba 12, ilisema kwamba shughuli zote za soka za ngazi ya juu zitasitishwa mara moja.

Haya yanajiri kufuatia mjadala uliotolewa na kamati hiyo baada ya kuteuliwa ofisini na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Michezo, Amina Mohamed.

Shughuli zilizosimamishwa ni pamoja na Ligi Kuu ya FKF, Ligi Kuu ya Kitaifa ya FKF, FKF Daraja la Kwanza, Ligi Kuu ya Wanawake ya FKF, na Ligi ya Divisheni ya 1 ya FKF ya Wanawake.

Kamati hiyo inatarajiwa kuwasiliana na vilabu na wadau wengine wa soka kabla ya kutoa mapendekezo zaidi.

Hata hivyo, ligi zinazoendeshwa chini ya matawi zitaendelea kama kawaida.

"Tunataka kuwahakikishia wapenzi wote wa soka ya Kenya kwamba kamati itahakikisha utendakazi mzuri wa shughuli zote za kandanda kote nchini na kwingineko," kamati hiyo ilisema.

Uahirisho ambao utaanza kutumika mara moja utaendelea kwa muda wa wiki mbili, kuanzia leo.

"Uamuzi umefikiwa ili kuhakikisha uratibu wa shughuli za ligi nchini kote,Kamati itakuwa ikishirikiana na vilabu na wadau wengine wa soka kwa wakati muafaka,"Ringera alisema katika taarifa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved