logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aina mpya ya kirusi cha Corona yatua Ulaya

Wataalamu mjini Geneva wataamua ikiwa kirusi hicho kinahitaji kutambuliwa kama ni hatari.

image
na Radio Jambo

Habari26 November 2021 - 20:43

Muhtasari


  • Wataalamu mjini Geneva wataamua ikiwa kirusi hicho kinahitaji kutambuliwa kama ni hatari

Ubelgiji imeripoti kisa cha kwanza cha aina mpya ya kirusi cha Corona barani Ulaya ambacho kwanza kigunduliwa nchini Afrika Kusini - huku Shirika la Afya Duniani likifanya mkutano maalum kuangazia umuhimu wake.

Wataalamu mjini Geneva wataamua ikiwa kirusi hicho kinahitaji kutambuliwa kama ni hatari.

WHO inasema itatoa mwongozo mpya baada ya mazungumzo lakini imeonya kwamba itachukua wiki kadhaa kubaini ikiwe kirusi hicho kivyoweza kuambukizwa na ikiwa chanjo itasalia kuwa na ufanisi dhidi yake.

Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen,iliwakumbusha watengenezaji kwamba kandarasi zao na EU inamaanisha lazima wabadili chanjo zao mara moja kwa kuzingatia kirusi hiki kipya.

Pia alisema kuwa safari zote za anga kwenda nchi zilizo na kirusi kipya cha corona zinapaswa kusitishwa.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved