logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vita vyazuka kanisani Kileleshwa kufuatia mzozo wa uongozi, 2 waliojihami kwa bunduki wakamatwa

Makasisi na waumini waligeuza kanisa la Lavington Methodist kuwa uwanja wa vita huku wakitupiana ngumi, mateke na maneno makali kufuatia mzozo kuhusu nani angeongoza kanisa ile.

image
na Radio Jambo

Habari04 December 2021 - 10:40

Muhtasari


•Kikundi kimoja cha waumini 60 kilichoongozwa na mchungaji anayeridhi uongozi Joseph Kanyamu kiliingia katika ofisi za kanisa kwa nguvu baada ya kuvunja mlango wa kioo wakiwa na nia ya kumtimua askofu Joseph Ntombura ambaye inasemekana muhula wake umetamatikana.

Kanisa

Vita vikubwa vilitanda katika kanisa moja iliyo eneo la Kileleshwa baada ya makundi mawili pinzani kutofautiana kuhusu uongozi wa kanisa.

Makasisi na waumini waligeuza kanisa la Lavington Methodist kuwa uwanja wa vita huku wakitupiana ngumi, mateke na maneno makali kufuatia mzozo kuhusu nani angeongoza kanisa ile.

Kulingana na DCI, kikundi kimoja cha waumini 60 kilichoongozwa na mchungaji anayeridhi uongozi Joseph Kanyamu kiliingia katika ofisi za kanisa kwa nguvu baada ya kuvunja mlango wa kioo wakiwa na nia ya kumtimua askofu Joseph Ntombura ambaye inasemekana muhula wake umetamatikana.

Wakati vita vilichacha mlinzi ambaye alishangazwa na waumini waliokuwa wamegeuka kuwa wahuni  alifahamisha polisi kutoka kituo cha Kileleshwa kuhusu kilichokuwa kinaendelea.

Polisi walipofika pale waliweza kuthibiti tukio na kukamata jamaa wawili kutoka kikundi cha mchungaji Kanyamu ambao walikuwa wamejihami kwa bastola aina ya Glock.

Wawili hao, Kisito Matete (43) na Peter Murasi (36)  walitiwa mbaroni baada ya kunyang'anywa batola zao na kupelekwa hadi kituo caa Kilimani.

Polisi wataendelea kulinda na kufuatilia kanisa hilo hadi wakati hali ya wasiwasi kati ya makundi hayo mawili itaisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved