logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wamunyinyi apasua mbarika kuhusu kilichomfurusha Ford K

Mbunge wa Kanduyi Wamunyinyi na mwenzake wa Tongaren Eseli Simiyu waliungana na kuunda chama kitakacho wasaidia kuleta pamoja watu wa magharibi.

image
na

Habari15 December 2021 - 11:38

Muhtasari


•Mbunge wa Kanduyi Wamunyinyi na mwenzake wa Tongaren Eseli Simiyu waliungana na kuunda chama kitakacho wasaidia kuleta pamoja watu wa magharibi.

•Kuunda chama kipya nchini hakujakuwa jambo geni vyama vingi vimevujwa uku vingine vipwa vikizaliwa

Nbunge wa Kanduyi MP Wafula Wamunyinyi wakati wa mazishi ya kakake Kizito wafula

 

 Mbunge wa Kandunyi Wafula Wamunyinyi amesema  uzinduzi wa chama chake kipya cha DAP-K siku ya  Jumanne  ulikuwa muhimu kwa kulinda jamii ya magharibi dhidi ya kutumiwa vibaya na wanasiasa wanaotaka kura zao.

Chama hicho kilizinduliwa katika ukumbi wa Bomas of Kenya baada ya mrengo wa Ford Kenya ambao   unaongozwa na Moses Masika Wetang’ula kukataa kuafikiana na waasi hao.

Mbunge huyo pamoja na mwenzake wa Tongaren Eseli Simiyu waliungana na kuunda chama cha DAP-K wakikusudia kukitumia  kuleta pamoja watu wa magharibi.

Akiwa kwenye mahojiano katika kituocha Citizen, Wamunyinyi alisema vyama vingine vimekuwa vikiwanyanyasa watu wa Magharibi na wametosheka  na hulka yao

“Chama kidogo kinachoongozwa na Musalia kimetumika kuwanyanyasa watu wa Magharibi na tumetosheka.Ni lazima waelewe; na  wajue kuwa tunaenda mashinani kuhakikisha haturuhusu watu wetu kutumiwa tena,”  Wamunyinyi alisema

Aliendelea kusema chama cha  Dap-k ni cha kidemokrasia ambacho kinasimamia umoja wa nchi na wangependa kuona jamii yenye usawa.

Kuunda chama kipya nchini sio  jambo geni  kwanivyama  vingi vimevujwa huku vingine vipwa vikizaliwa

 Wamunyinyi alitaja mzozo kati yake na Wetangula kama sababu kuu ya kugura chama cha Ford Kenya na kuunda kingine.

Walipohojiwa ni kwa nini chama kilichagua kutosimamisha mgombeaji urais mwaka ujao ili kuidhinisha kampeni ya Azimio la Umoja ya Raila Odinga, chama hicho kilisisitiza kuwa DAP-K ni chama changa ambacho hakina nia ya kuwasilisha ombi la urais kwa haki. kwa ajili yake.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved