logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Aliniacha baada ya kupata vyombo chafu jikoni,'Mwanamume asimulia masaibu ya ndoa yake

Wengi hupitia na kupigania ndoa yao, lakini wengi wao huchoka na kuwaacha wapenzi wao

image
na Radio Jambo

Habari07 January 2022 - 11:04

Muhtasari


  • Wengi hupitia na kupigania ndoa yao, lakini wengi wao huchoka na kuwaacha wapenzi wao, huku wakiendelea na maisha yao
sad man

Je sababu yako kuu ya kugura au kumuacha mke wako au kuachwa na mke wako kwenye ndoa yako ni ipi?

Wengi hupitia na kupigania ndoa yao, lakini wengi wao huchoka na kuwaacha wapenzi wao, huku wakiendelea na maisha yao.

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii jamaa mmoja aliwaacha wengi midomo wazi baada ya kufichua sababu kuu ambayo ilimfanya mke wake amuache.

"Mke wangu aliniacha mwezi wa Desemba mwaka jana baada ya kutoka sherehe na kupata kwamba sijaosha vyombo alikusanya virago vyake na kuenda kwao

Ilhali ata baada ya kuniambia ameenda kwao niliambiwa kwamba hajafika nyumbani, na ameniachia watoto 2, wiki jana alinipigia simu na kuniambia kwamba anataka kurudi tena, sijui nimwwambie nini kwani mwanamke kama huyu siwezi kuvumilia maisha naye, nimekuwa nikifanya mambo mengi na kuvumilia mengi lakini sasa amenifika kwenye koo, nahitaji ushauri kutoka kwa wanamitandao."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved