logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila ni tajiri lakini ni mchoyo - Ruto

Raila mara kadhaa ametilia shaka chanzo cha utajiri wa Ruto huku akihoji vile anatoa mamilioni ya pesa kama misaada kwa makundi tofauti wakati wa kampeni zake.

image
na Radio Jambo

Habari10 January 2022 - 04:53

Muhtasari


Alisema Raila anamiliki kampuni za mabilioni ya pesa lakini hawezi kuwasaidia wasiojiweza na maskini.

Ruto alisema Kenya iko tayari kwa kiongozi ambaye ana nia ya kuhakikisha kuwa kuna fursa sawa kwa raia wake wote bila kujali hali zao za kijamii.

Raila mara kadhaa ametilia shaka chanzo cha utajiri wa Ruto huku akihoji vile anatoa mamilioni ya pesa kama misaada kwa makundi tofauti wakati wa kampeni zake.

Ruto (kushoto) na Odinga (kulia), walikuwa 'maswahiba' wanaotarajia kusigana katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2022

Naibu rais William Ruto mwishoni mwa wiki alimsuta kiongozi wa ODM Raila Odinga kwa kukashifu wema wake wa kufadhili makundi mbali mbali na mazoea yake ya kutoa pesa.

"Kwa nini wanahangaika na mimi kutoa Shilingi 2 milioni; hizo ni pesa kidogo sana ambazo wanazo lakini ni wa choyo sana," Ruto alisema.

Alisema Raila anamiliki kampuni za mabilioni ya pesa lakini hawezi kuwasaidia wasiojiweza na maskini.

Raila mara kadhaa ametilia shaka chanzo cha utajiri wa Ruto huku akihoji vile anatoa mamilioni ya pesa kama misaada kwa makundi tofauti wakati wa kampeni zake.

Wakati huo huo, Ruto aliwataka wakazi wa Magharibi mwa Kenya kuunga mkono azma yake ya urais.

Alizungumza katika soko la Ekitale huko Kanduyi, kaunti ya Bungoma.

Alisema amejitolea kubadilisha maisha ya Wakenya wa kawaida.

Ruto alisema Kenya iko tayari kwa kiongozi ambaye ana nia ya kuhakikisha kuwa kuna fursa sawa kwa raia wake wote bila kujali hali zao za kijamii.

Aliahidi kupunguza gharama ya uzalishaji wa kilimo iwapo atachaguliwa kuwa rais.

Ruto alisema gharama ya sasa ya uzalishaji zinamnyanyasi mkulima.

“Tutahakikisha kuwa tunapunguza gharama ya ukulima ili wakulima wadogo wafurahie jasho la ukulima wao,” Ruto alisema.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved