logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Alichinjwa kama Ng'ombe,'Mkewe Isaac Juma asimulia jinsi mumewe alivyouawa

Alisema washambuliaji walikuwa tayari wametoroka kutoka nyumbani.

image
na Radio Jambo

Habari27 January 2022 - 10:04

Muhtasari


  • Mkewe shabiki mkongwe wa Harambee Stars Isaac Juma amesimulia jinsi mumewe aliuawa kwa kukatwakatwa

Mkewe shabiki mkongwe wa Harambee Stars Isaac Juma amesimulia jinsi mumewe aliuawa kwa kukatwakatwa.

"Tulikuwa tukila chakula cha jioni nyumbani kwetu na kabla ya kulala, tulisikia kondoo wakilia kwenye shamba letu," alisema.

Akizungumza na KTN siku ya Alhamisi, Farida alisema Juma aliondoka nyumbani kwenda kuangalia tatizo lilikuwa wapi.

"Lakini walipofungua mlango, wanaume hao walikuwa wakimngoja juu ya mti," alisema kwa njia ya kitamathali huku akielekeza kwenye mti uliokuwa nyuma yake.

"Alipiga mayowe kuomba msaada alipowaona wanaume hao. Niliposikia zogo, niliamka haraka na kumkuta mume wangu mikononi mwa washambuliaji," alisema.

Alisema washambuliaji walikuwa tayari wametoroka kutoka nyumbani.

“Alikuwa akikata shingo mithili ya mtu anayechinja ng’ombe, aliponiona naye alikimbia,” alisema.

"Aliniambia alikuwa na masuala ya ardhi katika eneo hilo, na ikitokea kifo chake, niwaambie mamlaka kwamba ni kwa sababu ya mgogoro wa ardhi."

Polisi walisema wamemkamata mshukiwa kuhusu shambulio hilo.

Maafisa wanaoshughulikia suala hilo walisema matokeo ya awali yameonyesha shambulio hilo lilitokana na mzozo wa ardhi katika eneo hilo.

Kutoka kwetu wanajambo Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved