logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Mhubiri Lucy Natasha na Prophet Carmel wafunga pingu za maisha katika harusi ya kitamaduni

Prophet Carmel ambaye ana asili ya Kihindi alimvisha Natasha pete ya uchumba mnamo mwezi Novemba mwaka jana.

image
na Radio Jambo

Habari30 January 2022 - 06:14

Muhtasari


•Prophet Carmel ambaye ana asili ya Kihindi alimvisha Natasha pete ya uchumba mnamo mwezi Novemba mwaka jana.

Mhubiri Lucy Natasha aolewa katika harusi ya kitamaduni

Mhubiri mashuhuri nchini Lucy Natasha na kipenzi chake Prophet Carmel kwa sasa ni mke na mume kirasmi baada yao kufunga pingu za maisha katika harusi ya kitamaduni iliyoandaliwa Jumamosi.

Wawili hao ambao wamekuwa kwenye mahusiano kwa kipindi kisichothibitishwa walipiga hatua hiyo muhimu maishani mbele ya familia na marafiki wachache waliokuwa wamealikwa.

Natasha alitumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kutangazia wafuasi wake kuhusu harusi yake huku akieleza ilikuwa siku ya kukata na shoka.

"'Mapenzi ni kitu kitamu, unapopata mwenzako bora, siku zako hujawa na furaha, furaha na utimilifu. Nyakati za furaha wakati wa Harusi yetu ya Kitamaduni." Natasha aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Prophet Carmel ambaye ana asili ya Kihindi alimvisha Natasha pete ya uchumba mnamo mwezi Novemba mwaka jana.

Mamia ya Wakenya wamejumuika mitandaoni kuwapongeza wawili hao wanapojiandaa kuanzisha familia pamoja.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved