logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wema Sepetu amfikisha mahakamani Aristostle kwa matamshi ya udhalilishaji

Mwanasheria wa Wema Sepetu ameeleza kwamba wameenda makamani kuhakikisha mteja wake amepata kulipwa  kutokana na maneno yaliyotolewa na Aristostle.

image
na

Habari01 February 2022 - 07:06

Muhtasari


•Mwanasheria wa Wema Sepetu ameeleza kwamba wameenda makamani kuhakikisha mteja wake amepata kulipwa  kutokana na maneno yaliyotolewa na Aristostle.

• Aristostle kisu chake kimotoni baada ya maneno aliyoyatoa kuhusu muigiaji maruufu nchini Tanzania  Wema Ssepetu, ambayo yalichukuliwa kama kudhalilisha jinsia ya  kike kwa jumla.

wema 5 (1)

Ni bayana sasa mwanahabari na mwandani wa Irene Uwoya , Aristostle kisu chake ki motoni baada ya maneno aliyoyatoa kuhusu muigiaji maruufu nchini Tanzania  Wema Ssepetu, ambayo yalichukuliwa kama udhalilishaji wa jinsia ya  kike kwa ujumla.

Wema Sepetu amemfikisha Aristostle  mahakamani baada ya kushauriana na wakili wake kuhusu matamshi ya mwanahabari huyo.

Kupitia kituo kimoja cha  radio nchini humo, wakili wa Wema Sepetu ameeleza kwamba wameenda makamani kuhakikisha mwigizaji huyo amepata kulipwa  kutokana na maneno ya udhalilishaji  yaliyotolewa na Aristostle.

Ikumbukwe Aristostle  alionyesha kujuta maneno yake na akajitokeza kumuomba msamaha muigizaji huyo. Msamaha wa mwanahabari huyo unaonekana kugonga ukuta, huku mwanasheria wa Wema akiwa ashamfungulia kesi mwanahabari huyo.

"Tunafuatilia kuona kwamba msanii wangu amepata kulipwa. kwa sababu ametukanwa, na watu walio na pesa, Irene ana pesa  natumai atamsimamia Aristotle na yeye amlipe mteja wangu. Msamaha aliyeomba Aristotle hufai kamwe kuitwa msamaha kwa sababu alijua vyema alichokuwa akitenda," alisema mwanasheria wa Wema Sepetu.

Kutokana na cheche za maneno na matusi ya mashabiki  yaliyotawala  ukurusu wa Aristostle imemlazimu kuchokonoa ukurusa wake wa instagram.

Ni kweli wazi kuwa chochote usemacho  kuhusu mtu mwingine kufikiria kabla ya kutenda usije ukajichimbia kaburi yako mwenyewe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved