logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tofauti' kati yangu na Mikel Arteta ilisababisha niondoke Arsenal -Pierre-Emerick Aubameyang

Kuondoka kwa Aubameyang kulikuja baada ya kuvuliwa unahodha wa Arsenal kufuatia utovu wa nidhamu.

image
na Radio Jambo

Habari04 February 2022 - 09:08

Muhtasari


  • Kuondoka kwa Aubameyang kulikuja baada ya kuvuliwa unahodha wa Arsenal kufuatia utovu wa nidhamu
Nahodha wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang.

Pierre-Emerick Aubameyang amesema "tofauti" kati yake na kocha wa Arsenal Mikel Arteta ilichangia uamuzi wake wa kuihama klabu hiyo na kujiunga na Barcelona.

Mshambulizi huyo wa Gabon alikamilisha uhamisho wa bila malipo kwenda Barca siku ya Jumatano baada ya kufungiwa nje ya kikosi cha The Gunners.

Kuondoka kwa Aubameyang kulikuja baada ya kuvuliwa unahodha wa Arsenal kufuatia utovu wa nidhamu.

"Nadhani ilikuwa shida upande wake tu [Arteta]," mchezaji huyo wa miaka 32 alisema wakati wa uzinduzi wake Nou Camp siku ya Alhamisi.

"Alifanya uamuzi. Siwezi kusema mengi zaidi. Hakuwa na furaha, japo nilikuwa mtulivu sana lakini ndio hivyo tena."

Aubameyang aliachiliwa kuondoka Arsenal siku ya Jumatatu bila kujitokeza kufuatia suala la kinidhamu mwezi Disemba.

Mshambulizi huyo wa zamani wa Borussia Dortmund hapo awali mnamo mwezi Machi alikosa mechi ya ushindi dhidi ya Tottenham kaskazini mwa London kwa sababu ya "ukiukaji wa itifaki ya kabla ya mechi".

Lakini ana matumaini ya kufufua mchezo wake huko Barca kabla ya mechi ya kwanza dhidi ya Atletico Madrid siku ya Jumapili.

"Ni kweli kwamba ilikuwa miezi migumu na nadhani soka huwa na mambo haya wakati mwingine," aliongeza Aubameyang.

"Lakini kama itabidi niseme kitu kuhusu mada hii [kuondoka Arsenal], ni kwamba sikuwahi kufanya lolote baya kwa upande wangu, lakini nadhani hayo yamepita na ninataka kufikiria kuhusu hali yangu ya sasa."

Aubameyang alifunga mabao 92 katika mechi 163 alizochezea Arsenal kufuatia uhamisho wake wa pauni milioni 56 kutoka Dortmund Januari 2018, akiwasaidia The Gunners kushinda Kombe la FA 2020 na kumpa Arteta medali ya fedha katika msimu wake wa kwanza kushikilia usukani.

Mkataba wake Barcelona utaendelea hadi Juni 2025 na unajumuisha chaguo la kukubali kuondoka mnamo Juni 2023, pamoja na kifungu cha ununuzi cha euro milioni 100 (£83.4m).

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved