logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tukutane kwa bar' Iyanii atoa kibao cha Valentines

yanii ambaye ni msanii anayeibukia kwenye sanaa ya muziki  mwaka jana alitoa  kibao cha Pombe,ambacho kilichezwa kwenye tamasha mbalimbali za burudani.

image
na

Habari07 February 2022 - 05:39

Muhtasari


•Msanii Iyanii ametoa kibao kipya ambacho kinajikita kwenye siku ya wapendanao ambacho  kinachojulikana kama ‘Tukutane kwa Bar.

•Iyanii ambaye ni msanii anayeibukia kwenye sanaa ya muziki  mwaka jana alitoa  kibao cha Pombe,ambacho kilichezwa kwenye tamasha mbalimbali za burudani.

Iyanii

Msanii Iyanii ametoa kibao kipya 'TTukutane kwa Bar' ambacho kinazungumzia siku ya wapendanao.

Iyanii ambaye ni msanii anayeibukia kwenye sanaa ya muziki  mwaka jana alitoa  kibao cha Pombe,ambacho kilitesa sana katika maeneo mbalimbali ya burudani.

‘Pombe’  ni mojawapo  ya vibao vya Iyanii ambavyo vilitokea kupendwa sana na wakenya hasa katika  msimu wa Krismasi.

Miongoni mwa vibao ambavyo msanii huyo ametoa na zinafanya vizuri ni  kama; Furaha na Pombe na cha hivi majuzi tukutane kwa bar.

‘Tukutane kwa bar’ ni kibao ambacho kinazungumzia wale watu hawana wapenzi hasa mwezi huu wa mapenzi, anawashauri badala ya kujililia kwenye vitanda vyao wajitokeze kwenye virabu  wapige sherehe pamoja kuepusha upweke unaokumba mtu wakati hana mpenzi.

Lengo la wimbo huo ni kuleta mashabiki pamoja na kusherekea siku hio muhimu kwa wapendao na kufanya wengi kuwa na tabasamu nyusoni badala  ya kukaa kwenye kitanda usiku upweke ukiwa kumba si haba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved