logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mlinzi wa West Ham Kurt Zouma tabaani baada, Adidas yajiondoa

Video hio akimpiga teke paka wake ilisambazwa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii

image
na

Habari10 February 2022 - 04:16

Muhtasari


•Mchezaji wa timu ya West Ham, Kurt Zouma amejipata pabaya baada ya kanda za video zilizomwonyesha akipiga  teke paka wake kwenye malazi yake.

 

Kurt Zouma

Mchezaji wa timu ya West Ham, Kurt Zouma amejipata pabaya baada ya kanda za video zilizomwonyesha akipiga  teke paka wake kwenye malazi yake.

Zouma alisajiliwa na West Ham kutoka timu ya Chelsea ingawa kwa mkopo, tangu video hiyo kuonekana kwenye mitandao, wanamitandao wamekuwa  na maoni kinzani huku wengine wakitaka afikishwe mahakamani.

Siku ya Jumatatu  paka wawili ambao mchezaji huyo alikuwa amefuga nyumbani kwake walichukuliwa na shiriki la kulinda wanyama nchini Uingereza RSPCA. Hii ni baada ya picha kuonekana akimpiga teke mmoja wa paka wake.

Video ya Mfaransa huyo akimpiga teke paka wake ilisambazwa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii na kuvutia macho wapenzi wa wanyama na mamlaka  inayosimamia wanyama kuanza  kampeni za kumkashifu kwenye mitando ya kijamii.

Ingawa Kurt Zouma aliomba msamaha, timu ya West Ham imempiga faini kwa kosa alilotenda siku hiyo.

Kampuni ya vifaa vya spoti Addidas pia imeondoa ufadhili wake kwa mchezaji huyo kutokana na tukio hilo.

 Katika Taarifa Jumatatu, Jumuiya ya Kifalme ya Kulinda Wanyama ililaani kitendo cha Zouma huku ikibainisha kuwa wamemchukua paka hao.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved