logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nandy apongeza waliofanikisha hafla ya kulipiwa mahari

Amepongeza mashabiki wake kwa  kufanikisha hafla ya kulipiwa mahari.

image
na

Habari22 February 2022 - 05:45

Muhtasari


• Nandy almaarufu The African Princess amepongeza mashabiki wake kwa  kufanikisha hafla ya kulipiwa mahari na mume wake Billnass.

• Inaarifiwa kuwa Billnas alitumia shilingi milioni 18 za Kitanzania kulipa mahari.

Mwanamuziki na muigizaji  wa kike Nandy almaarufu The African Princess amepongeza mashabiki wake kwa  kufanikisha hafla ya kulipiwa mahari na mumewe Billnass.

Mwanamuziki huyo alilipiwa mahari  na Billnas siku ya Jumapili  ambapo ilikuwa ni sherehe kubwa nyumbani kwa akina Nandy.

 Siku ya Jumatatu, wawili hao walichapisha kanda ya video ambayo ilikuwa inaonyesha Bilnass akipiga magoti chini na kumvisha pete ya uchumba  mwamuziki huyo ambapo  inaarifiwa kuwa Billnas alitumia milioni 18 za Kitanzania kulipa mahari.

Kupitia ukurusa wa instagram Nandy amepongeza wote waliofanikisha siku hiyo na kuwa ya kuvutia.

“ Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wale wote walio kuwa na sisi siku yetu ya mahari jana neno ASANTE ndilo tunaweza kusema! Vyombo vya habari vilivyotangaza haabari hizo ndani na nje ya nchi hatuna cha kulipa kwa msaada wenu,”Alisema Nandy.

Vilevile aliomba msamaha kwa mashabiki ambao walikuwa na matamanio ya kufika kwenye sherehe hizo lakini hawakuweza kwa sababu ambazo hakuziweka wazi.

“Pia tunaomba radhi kwa wale ambao walitamani kuwa nasi pamoja Jana na haikuwezekana kwa Sababu ziliko nje ya uwezo wetu na wao nyinyi nyote mna umuhimu kwetu siku special na kubwa inafika tutajumuika wote. MUNGU ni Mwema sana na imefanyika kuwa kweli!”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved