logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nandy ashindwa kuvumilia upweke baada ya Billnas kwenda Dubai

Wiki jana Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba nyumbani kwao Nandy

image
na

Habari04 March 2022 - 10:11

Muhtasari


•Wiki jana Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba nyumbani kwao Nandy, huku wakifichua kwamba ndoa rasmi haitopita mwezi wa sita.

The Africa princess 'Nandy'

Mwanamuziki wa kike Nandy amefunguka makubwa baada kuandika ujumbe  kwenye ukurasa wa mpenziwe kuwa anataka arudi nyumbani haraka.

Mpenzi wa Nandy, Billnass aliondoka nchi ya Tanzania kuekelekea Dubai ambapo inasemekana ameenda kwa shughuli ya kibiashara.

Wiki jana Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba nyumbani kwao Nandy, huku wakifichua kwamba ndoa rasmi haitopita mwezi wa sita.

Billnass alimjibu Nandy kwa kumueleza kuwa anatafuta vazi ambalo atavaa siku ya harusi ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa na Mashabiki wa wiwili hao.

"Nandy nakutafutia gauni la Harusi, Maana hizi vita zinanichanganya tunaweza fungia ndoa kwa kifaru,"alisema Billnas.

Ni hivi majuzi Nandy amekanusha madai kwamba amechepuka baada ya mtangazaji wa shirika la habari nchini humo, kumfumania usiku akisindikizwa kwenye gari na mwanamume mwingine ambaye Mwijaku alibaini si yule ambaye amemchumbia juzi, Billnass.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved