logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatimaye Diamond aweka wazi kirefu cha EP ya #FOA

Diamond ameweka wazi maana ya FOA ni First of All.

image
na Radio Jambo

Habari08 March 2022 - 04:21

Muhtasari


• Hatimaye msanii Diamond ameweka wazi maana ya jina la EP yake ya FOA  inayotarajiwa kutoka Machi 11.

Hatimaye msanii Diamond Platnumz ameweka wazi kirefu cha EP yake ambayo mwishoni mwa wiki jana aliitangaza kwa kutoa kifupi chake kuwa FOA.

Diamond ametangaza Jumatatu kwamba kirefu cha jina la EP yake ambayo inatarajiwa kutoka Machi 11 ni First Of All, kwa maana kwamba ni Kabla ya Yote, wengi wakisema maana hii inaonesha uhalisia wenyewe kwani ni EP yake ya kwanza kabisa tangu aingie kwenye muziki Zaidi ya miaka kumi iliyopita.

Wiki jana Diamond alipakia picha za kifupi cha jina la EP hiyo ambayo ilitembezwa mitandaoni chini ya alama ya reli ya #FOA na kuwataka wafuasi wake na mashabiki wake kung’amua kirefu chake ambapo wengi walitatizika kichwa kwa ubashiri tofauti tofauti za kuchekesha na zingine za kukejeli.

Lakini almradi wenye midomo walishasema kwamba hata usiku uwe mrefu vipi bado kutapambazuka tu, basi Jumatatu kulipambazuka na msanii huyo akalitatua hilo kwa kuweka wazi kirefu chake.

Kinachosubiriwa na wengi sasa ni kujua idadi ya ngoma ambazo EP hiyo inasheheni lakini hili bila shaka litabainika tarehe 11 mwezi huu ambapo pia wengi wanatarajia kuipata radha kamili na iliyotukuka ya muziki wa nguli huyo wa bongo fleva kama ilivyokuwa kawaida yake miaka ya nyuma.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved