logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muhubiri Ng'ang'a asema haya kuhusu video iliyooenea akimuombea msanii Rose Muhando

Ng'ang'a anasema watu waliiondoa video hiyo nje ya muktadha kwani ilihusisha mtu mashuhuri.

image
na Radio Jambo

Habari22 March 2022 - 20:16

Muhtasari


  • Mchungaji Ng'ang'a hatimaye amezunumzia video inayomuonyesha akitoa pepo kutoka kwa msanii wa Tanzania, Rose Muhando

Mchungaji Ng'ang'a hatimaye amezunumzia video inayomuonyesha akitoa pepo kutoka kwa msanii wa Tanzania, Rose Muhando.

Video hiyo iliacha ndimi zikitetereka baada ya kugonga mitandao ya kijamii na yote kwa sababu zisizo sahihi.

Katika mahojiano ya kipekee na Mpasho, Ng'ang'a anasema watu waliiondoa video hiyo nje ya muktadha kwani ilihusisha mtu mashuhuri.

"Sina shida na Rose Muhando. Kuna wakati alinipigia simu na kunishukuru akisema amepona. Naombea watu mbalimbali.

Muhando ni nani? Yeye ni mtu kama mtu mwingine yeyote kwa nini anamlenga. Kwa nini usiulize kuhusu watu wanaougua saratani ambao nimewaombea?

Tunapoenda kwenye huduma kila mtu ni kondoo. Alivuma tu kwa sababu yeye ni msanii. Video ilivuma kimakosa," Alieleza Ng'ang'a

Muhubiri huyo aliendelea kutoa mfano wa mwanamke aliyetokwa na damu kwa miaka mingi na licha ya yote yesu alimponya hadharani, huku akisema kwamba hamna mtu mdogo wala mkubwa mbele ya Munu.

"Mbele za Mungu, hakuna mkubwa zaidi ya mwingine. Hata Yesu alimponya mwanamke aliyetokwa na damu kwa miaka mingi hadharani ikiwa kuna kamera wakati huo tungemuona. hakumuombea hadharani watu wangejuaje kuwa mtu wa aina ya Muhando anaweza kuugua na kupona?

Sasa anajulikana zaidi kuliko hapo awali."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved