logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Umejizolea mali ambayo wanaume wa miaka 69 wanatamani" Akothee amsifia Betty Kyalo

Akothee alisema kwamba mtangazaji na mfanyibiashara huyo hajabarikiwa kwa urembo tu ila kwa hekima pia.

image
na Radio Jambo

Habari23 March 2022 - 05:28

Muhtasari


•Akothee amesema kwamba mtangazaji huyo tayari ameweza kujipatia utajiri mkubwa akiwa na umri wa ujana tu.

•Akothee alisema kwamba mtangazaji na mfanyibiashara huyo hajabarikiwa kwa urembo tu ila kwa hekima pia.

Mwanamuziki na mjasiriamali Esther Akoth almaarufu Akothee amempongeza mtangazaji mashuhuri Betty Kyallo kwa mafanikio makubwa ambayo ameweza kujizolea.

Akothee amesema kwamba mtangazaji huyo tayari ameweza kujipatia utajiri mkubwa akiwa na umri wa ujana tu.

"Msichana mdogo mwenye ndoto kubwa na mafanikio makubwa. Katika umri wa miaka 30 tayari umejizolea mali ya kutosha ambayo wanaume wengi katika miaka 69 hutamani tu," Akothee alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Mama huyo wa watoto watano alimtakia Betty Kyallo kheri za siku ya kuzaliwa anapotimiza miaka 33. 

Akothee alisema kwamba mtangazaji na mfanyibiashara huyo hajabarikiwa kwa urembo tu ila kwa hekima pia.

"Wewe ni malkia kweli! Kheri za siku ya kuzaliwa Betty Kyallo mwituasa," Akothee aliandika.

Betty alipendezwa na ujumbe wa Akothee na kumshukuru huku akimtaja kama dadake mkubwa na mwanamke mzuri.

Mtangazaji huyo alisherehekea siku yake ya kuzaliwa mnamo Machi 15.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved