Bintiye aliyekuwa Seneta wa Kaunti ya Kakamega Boni Khalwale alikuwa miongoni mwa watahiniwa 1,214,301 waliofanya mtihani wa KCPE wa 2021.
Saa chache baada ya kutangazwa rasmi kwa matokeo ya mtihani wa KCPE, Khalwale alienda kwenye Twitter na kusambaza ujumbe wa shukrani kufuatia utendakazi wa kuvutia wa bintiye.
"Familia yangu na mimi, kwa njia 1000 maalum tunamshukuru Mungu, walimu na wasio walimu wa Shule ya Msingi ya Malinya na Shule ya Kakamega Hill Junior kwa 402!" Khalwale aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Melissa Khamwenyi Khalalwe, bintiye Boni, alijizolea 402.
Kulingana na matokeo yaliyoshirikiwa na Khalwale, Melissa Khamwenyi Khalwale wa nambari 37615027005 alipata matokeo kama yafuatayo: "ENG 86-A, KIS 83-A, MAT- 83-A, SCI 66-B, SSR 84-A". Alama zote zinaongeza hadi alama 402.
My family & I, in 1000
— Dr Boni Khalwale, CBS (@KBonimtetezi) March 28, 2022
special ways thank God, the teaching & non teaching staff of Malinya Pr. School & Kakamega Hill Junior School for the 402!
MELISSA KHAMWENYI KHALWALE INDEX: 37615027005 ENG 86A KIS 83A KSL = = MAT 83A SCI 66B SSR 84A TOTAL 402 KNEC HELPLINE 0800724900 pic.twitter.com/CCtQSbD5rF
Katika matokeo yaliyotolewa, mwanafunzi wa kwanza, Bruce Mackenzie alijizolea alama 428