logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafahamu vipusa waliowahi kutoka kimapenzi na Harmonize

Sarah alimtema msanii huyo baada ya kugundua kwamba alikuwa amecheza karata nje ya ndoa.

image
na Radio Jambo

Habari30 March 2022 - 06:28

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuja kutambulika takriban mwongo mmoja uliopita na tangu wakati huo mahusiano yake yamekuwa hadharani.

•Siku za hivi majuzi Harmonize ameonekana akijaribu kumbembeleza mwigizaji huyo amrudie huku akisema anajuta kumkosea.

Kwa miaka mingi, maisha ya mahusiano ya staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize yamekumbwa na utata si haba.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuja kutambulika takriban mwongo mmoja uliopita na tangu wakati huo mahusiano yake yamekuwa hadharani.

Mahusiano ya kwanza ya Harmonize kujulikana hadharani yalikuwa na mwanamitindo Jacqueline Massawe Wolper.

Wawili hao walichumbiana kati ya mwaka wa 2016 na 2017 kabla yao kutengana katika hali tatanishi.

Wolper alimnyooshea Harmonize kidole cha lawama baada ya mahusiano yao kugonga ukuta huku akimshtumu kwa kukosa uaminifu katika ndoa.

Hata hivyo, takriban miaka miwili iliyopita, Harmonize alijitokeza kupuuzilia mbali madai hayo na kudai kwamba Wolper alikuwa na mazoea ya kutoka nje ya ndoa mara kwa mara.

Harmonize alisema Wolper hakuheshimu mipaka ya mahusiano yao na hata aliwahi kummezea mate aliyekuwa bosi wake katika Wasafi, Diamond Platnumz.

Jacque Wolper

Baada ya kutengana na Wolper, Harmonize alijitosa kwenye mahusiano na mlimbwende kutoka Italia, Sarah Michelotti.

Wawili hao walichumbiana kati ya 2017 na 2020 ambapo waliamua kuenda njia tofauti. Huba lilikuwa limekolea kwenye ndoa yap ya takriban miaka minne ila haikuweza kudumu.

Sarah alimtema msanii huyo baada ya kugundua kwamba alikuwa amecheza karata nje ya ndoa na hata kupata mtoto na mwanadada mwingine.

Mwaka jana, Harmonize alikiri kumcheza Sarah alipokuwa amesafiri kwenda kwao Italia na katika harakati hiyo akampachika mimba mwanadada aliyejihusisha naye.

Harmonize na aliyekuwa mpenzi wake Sarah Michelotti

Official Shanteel, kama anavyojitambulisha Instagram ndiye mwanadada ambaye Harmonize alitoka naye kimapenzi na kupata naye mtoto mwaka wa 2019.

Harmonize alimficha mwanawe kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi saba na hatimaye kumfichua  hadharani Desemba, 2020.

Ufichuzi wa Harmonize ulizua ugomvi kati yake na Sarah na kuchangia kutengana kwao.

Baada ya Harmonize kutemwa na Sarah aliingia kwenye  mahusiano mengine na mwigizaji Fridah Kajala Masaja.

Wawili hao walichumbiana kwa kipindi kifupi mwaka wa 2021. Waliweka mahusiano yao wazi mwezi Februari, 2021 ingawa tayari walikuwa wameanza kuchumbiana awali kabla ya kujitokeza.

Harmonize na Frida Kajala

Takriban miezi miwili tu baada yao kujitokeza kama wapenzi mahusiano yao yalifika kikomo katika hali tatanishi.

Walipokuwa kwenye mahusiano, Harmonize na Kajala walikuwa wamechora tatoo za majina yao kama ishara ya mapenzi makubwa kati yao. Hata hivyo wote walizifuta tatoo hizo baada ya kutengana.

Siku za hivi majuzi Harmonize ameonekana akijaribu kumbembeleza mwigizaji huyo amrudie huku akisema anajuta kumkosea.

Novemba mwaka jana, Harmonize alitambulisha kipenzi chake kipya kutoka Australia, Briana Jai. Konde Boy alimtangaza Briana kama malkia mpya kwenye ufalme wake huku akiahidi  kumpenda na kumlinda.

Harmonize na Briana

Wawili hao hata hivyo walitangaza kutengana kwao hivi majuzi baada ya kuwa pamoja kwa takriban miezi mitano.

Briana alifichua  kuwa vipaumbele vyao katika maisha vilikosa kuwiana na ndiposa wakaafikiana kutengana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved