logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize ampa Diamond tuzo baada ya kushinda tuzo ya mwanamuziki bora wa kiume 2021

Hii ni baada yakutoka kwenye lebo ya Wasafi na kuanzisha label yake ya Konde Music.

image
na Radio Jambo

Habari03 April 2022 - 05:02

Muhtasari


  • Harmonize ampa Diamond tuzo baada ya kushinda tuzo ya mwanamuziki bora wa kiume 2021
Instagram, KWA HISANI

Harmonize ni msanii maarufu wa Kitanzania wa Bongo anayejulikana kwa nyimbo zake zinazovuma na video zake bora.

Ni baba wa msichana mmoja mrembo aitwaye Zuu Konde. Harmonize ni miongoni mwa msanii nchini Tanzania anayeishi maisha ya kifahari kwani kutokana na wadhifa wake inaonekana .

Yeye ni mshawishi wa chapa, balozi wa chapa, mwanamitindo, Mkurugenzi Mtendaji, mfanyabiashara, mwandishi wa nyimbo, mwimbaji wa nyimbo.

Harmonize kwa muda wa miaka mitatu iliyopita hajakuwa akishirikiana na bosi wake wa zamani ambaye aliunga mkono muziki wake alipoanza Diamond Platnumz .

Hii ni baada yakutoka kwenye lebo ya Wasafi na kuanzisha label yake ya Konde Music.

Hata hivyo jana Harmonize alionyesha kuwa na maelewano mazuri naye alipokuwa akifanya shoo. Alisimama na kumwita diamond kuwa msanii bora zaidi Tanzania.

Alisema kuwa anajua kuwa hana maelewano naye lakini jembe linapaswa kuitwa jembe.

Huku akituzwa tuzo ya kuwa mwanamuziki bora wa kiume mwaka wa 2021, alikabidhi tuzo hilo kwa msanii Diamond huku akisema sio vyema kubeba tuzo tatu ilhali Diamond hajapata tuzo yeyote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved