logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mrengo wa Ruto waikosoa bajeti ya 2022-23, Mbunge Ndindi Nyoro asema takwimu ni za uongo

Ndindi Nyoro - “Hii bajeti iko mbali sana na mwananchi wa kawaida nac kama nilivyoshikilia hapo awali, bajeti hii iko na mapungufu mengi sana"

image
na Radio Jambo

Habari07 April 2022 - 15:25

Muhtasari


• “Hii bajeti iko mbali sana na mwananchi wa kawaida nac kama nilivyoshikilia hapo awali, bajeti hii iko na mapungufu mengi sana" - Ndindi Nyoro

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro

Mrengo wa Kenya Kwanza kama ilivyotarajiwa tayari umeikosoa vikali bajeti ya mwaka 2022-23 iliyosomwa bungeni Alhamis na Waziri wa fedha Ukur Yatani.

Akizungumza nje ya bunge pindi baada ya bajeti hiyo kusomwa, mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro alisema bajeti hiyo iko mbali sana na maslahi ya mwananchi wa kawaida na kuzikosoa takwimu zote za Ukur Yatani kuwa mambo ya kufikirika tu wala hayana mashiko yoyote.

“Hii bajeti iko mbali sana na mwananchi wa kawaida nac kama nilivyoshikilia hapo awali, bajeti hii iko na mapungufu mengi sana. Takwimu ambazo alipatiana kulingana na ukuaji wa GDP wala haziendani kabisa. Mwaka wa 2013, GDP ya kenya ilikuwa takribani dola bilioni 55 (KSH 6.3T). Mwaka jana kama utairejelea hotuba yake, alidai kwamba GDP ya Kenya ilikuwa takribani dola bilioni 100 (KSH 11.5T), halafu leo anasema kwamba GDP ya Kenya iko dola bilioni 135 (KSH 15.4T), hiyo inamaanisha nini? Kwamba kama mwaka jana ilikuwa dola bilioni 100, na sasa hivi n idola bilioni 135, basi uchumi wa taifa umekuwa kwa kasi ya asilimia 35, kama si hivyo basi itakuwa kulikuwepo na mambo fulani ambayo tulifichwa,” alisema Nyoro.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved