logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rotimi afurahisha wanamitandao kwa kumfunza mwanawe jinsi ya kuomba

Rotimi - “Tangulia na ungoza kama mfano. Waanzishe mapema na kumjua Mungu, kuwa na maongezi na Mungu,”

image
na Radio Jambo

Habari07 April 2022 - 07:53

Muhtasari


• “Tangulia na ungoza kama mfano. Waanzishe mapema na kumjua Mungu na pia jinsi ya kuwa na maongezi na Mungu,” aliandika Rotimi kwenye Instagram yake.

Rotimi na mwanwe wakiwa katika sala

Mpenzi wa aliyekuwa mtangazaji na mwanamuziki wa Tanzania Vanessa Mdee, Rotimi kutokea Marekani ameteka mtandao wa Instagram baada ya kupakia picha akiwa na mwanawe ambapo anamfunza jinsi ya kupiga sala na kuomba Mungu.

Mwanamuziki Rotimi ambaye alimuoa Vanessa Mdee baada ya mwanamama huyo kutengana na aliyekuwa mpenzi wake mwanamitindo na msanii Juma Jux alipakia picha hiyo na kuifuatisha kwa maneno kwamba ni vizuri kuwafunza watoto masuala ya uchamungu wangali bado wadogo.

“Tangulia na ungoza kama mfano. Waanzishe mapema na kumjua Mungu na pia jinsi ya kuwa na maongezi na Mungu,” aliandika Rotimi kwenye Instagram yake.

Mashabiki wengi waliotoa maoni yao kwenye post hiyo wamemmiminia sifa kochokocho msanii huyo kwa kuonesha picha nzuri ya kumfunza mtoto mdogo njia za Mungu hata kabla ya kutinga mwaka mmoja.

Katika mahojiano fulani mwezi mmoja uliopita, Rotimi alifunguka jinsi anavyojisikia kuwa baba na mazingira yalivyo katika shughuli nzima ya ulezi wa mwanawe.

Kwangu huo ni wakati wa kupumua na kuwa na familia yangu na kuangazia mambo yangu mazuri ambayo najali zaidi. Borake ananiona na kuona jinsi tulivyo na kusoma kadri iwezekanavyo, huo ni wakati muhimu zaidi kwangu. Ni vizuri kuona akikua kila siku” Rotimi alisema katika mahojiano kuhusu ulezi wa mwanawe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved