logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(Screenshot) Anerlisa aeleza jinsi mpenzi wake anamdekeza kwa mapenzi

Baada ya kutengana na Ben Pol, Anerlisa amedokeza kwamba mpenzi wake mpya anamdekeza kama yai

image
na Radio Jambo

Habari08 April 2022 - 09:26

Muhtasari


• Anerlisa Muigai aliachana na msanii Ben Pol siku chache baada ya kufanya harusi ya Kikatoliki.

• Kando na kuwa mrithi wa Keroche, ana kampuni yake binafsi inayojihushisha na masuala ya kupakia maji kwa jina la Nero.

Mrithi wa Keroche, Anerlisa Muigai

Baada ya kuachana na mwanamuziki kutoka Tanzania, Ben Pol, mrithi wa kampuni ya kutengenezxa vileo Keroche Breweries, Anerlisa Muigai hatimaye amepata wa kumpa shavu la mapenzi na amani ya moyo na nafsi.

Mwanamke huyo ambaye kuachana kwake na Ben Pol kulijiri siku chache tu baada ya ndoa takatifu kulimsababishia msanii huyo kuvunjika moyo vibaya sana mpaka kubadilisha dini kutoka ya Kikristu kuelekea ile ya Kiislamu.

Anerlisa ambaye pia kando na kuwa mrithi wa Keroche, ana kampuni yake binafsi inayojihushisha na masuala ya kupakia maji kwa jina la Nero.

Katika siku za hivi karibuni, Anerlisa amekuwa akiwatania wanamitandao kuhusu mpenzi wake mya ambaye alidinda sana kutambulisha uso wake kwa ‘mashemeji’ wa mitandaoni. Alikuwa anapakia picha za pamoja huku akiwa amemficha uso kweli kweli kama siri lakini wakati mmoja juzi kati hapa alionesha video ya mpenzi huyo wake wakati walikuwa katika hafla moja ya kusherehekea siku ya kuzaliwa ya Rafiki yake.

Ijumaa Anerlisa amepakia ‘meme’ kwenye Instagram yake ikiwa na mkono unaolishikilia yai kwa mtindo wa kudekeza vile ambapo inafuatishwa na maneno kwamba inaashiria kwa uhalisia jinsi mpenzi wake mpya anavyomdekeza na kumhendo kwa mapenzi yasiyojua kufa.

“Picha muhali sana inayotoa maelezo jinsi mpenzi wangu anavyonidekeza na kunihendo,” maneno hayo yanasema.

Anerlisa ambaye kampuni yao ya vileo Keroche imekuwa na mfarakano mkali na mamlaka ya ukusanyaji kodi, KRA kutokana na malimbikizi ya madeni ya ushuru alidokeza kwamba uamuzi wake wa kuhamia jijini Nakuru ni kutokana na kwamba mji huo una amani sana na amani ndio kama kitu kipya ndani yake anachokienzi sana.

screenshot

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved