logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneta Kihika apuuzilia mbali madai ya kuwa jasusi wa Jubilee katika UDA

Ameshikilia kuwa yuko katika chama cha UDA na anaunga mkono azma ya naibu rais William Ruto kuwania urais.

image
na Radio Jambo

Habari09 April 2022 - 05:55

Muhtasari


•Kihika alisema amewasamehe wale walioeneza ripoti hizo akisema kuwa ni mambo ya kawaida katika msimu wa kisiasa.

•Kihika hata hivyo ameshikilia kuwa yuko katika chama cha UDA na anaunga mkono azma ya naibu rais William Ruto kuwania urais.

Seneta wa kaunti ya Nakuru, Susan Kihika amepuuzilia mbali madai kuwa yeye ni jasusi wa Jubilee katika chama cha UDA.

Katika  taarifa yake ya Ijumaa jioni, Seneta huyo wa muhula wa kwanza alikanusha madai hayo na kusema kuwa ya ni ya kipuuzi.

"Waah nimeshutumiwa kwa uwongo kwa mambo mengi katika taaluma yangu ya kisiasa lakini sijawahi kuwa jasusi wa Jubilee katika UDA, haithuru (haijalishi)," alisema.

Kihika alisema amewasamehe wale walioeneza ripoti hizo akisema kuwa ni mambo ya kawaida katika msimu wa kisiasa.

"Ni msimu wa kisiasa wa kiasi cha hali ya juu ambapo chochote kinafanyika. Lakini ni sawa. Nimewasemehe. Mungu mbele," alisema.

Hapo awali, Mbunge wa Naivasha, Jane Kihara alimshutumu Kihika kwa kukutana na viongozi wa Chama cha Jubilee usiku na kuwaambia mambo ya ndani ya UDA.

"Seneta Susan Kihika hajasema ukweli na anaungana na wapinzani wetu wa kisiasa katika Jubilee Party ili kuhakikisha kwamba ni wagombeaji anaopendelea pekee wanapita," Kihara alisema.

Alidai mgombea huyo wa Ugavana wa Nakuru anamuunga mkono mpinzani wake katika nafasi ya ubunge wa Naivasha, John Kihagi wa Jubilee.

Kihika hata hivyo ameshikilia kuwa yuko katika chama cha UDA na anaunga mkono azma ya naibu rais William Ruto kuwania urais.

"Kwa kuondoa mashaka, hapa ndio tuko! Na hatusongi! Puuza propaganda ghushi za wanablogu waliokata tamaa! Ruto rais wa 5," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved