logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kura ya maoni: Nani anafaa kuwa mgombea mwenza wa William Ruto?

Musalia Mudavadi ameongoza orodha ya viongozi wanaopendekezwa kuwa wagombea wenza wa William Ruto.

image
na Radio Jambo

Habari21 April 2022 - 12:27

Muhtasari


• Wanasiasa mbalimbali wamependekezwa kuwa naibu wa William Ruto.

• Asilimia kubwa ya viongozi hao ni kutoka eneo la Mlima Kenya.

Huku siku rasmi ya uchaguzi ikizidi kukaribia kwa kasi, nafasi ya mgombea mwenza wa William Ruto inazidi kuwa kitendawili kikubwa.

Viongozi mbalimbali wamependekezwa kuchukua nafasi hiyo huku asilimia kubwa ikiwa kutoka eneo la Mlima Kenya.

Musalia Mudavadi anaongoza orodha hiyo kwa asilimia 24.2 huku mbunge wa Mathira Rigathi Gachagua anafuata kwa asilimia 20.2.

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro anachukua nafasi ya tatu kwa asilimia 11.3 huku Martha Karua akifunga nne bora kwa asilimia 10.5.

Mbunge wa Gatundu kusini na kiongozi wa Chama cha Kazi, Moses Kuria ni wa tano kwa asilimia 6.5.

Huku siku rasmi ya wagombea wa kiti cha urais kutangaza wagombea wenza ikiwa Aprili 28, naibu rais William Ruto amesema kwamba atakuwa anaandaa mkutano wiki kesho ili kufanikisha mchakato wa kutafuta atakayekuwa mgombea mwenza chini ya muungano wa Kenya Kwanza.

Aidha, kumekuwa na tetesi nyingi kutoka kwa viongozi mbalimbali kwamba iwapo Ruto atashinda uchaguzi huo lazima naibu wakeatoke katika eneo la kati mwa Kenya.

Wengine pia wamedadisi kwamba Ruto anapaswa kuchagua mgombea mwenza wa jinsia ya kike. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved