logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mike Tyson amrushia ngumi abiria mwenzake ndani ya ndege baada ya kurushiwa chupa

Tyson alimpiga abiria mwenzake ambaye alimchokoza bila sababu.

image
na Radio Jambo

Habari23 April 2022 - 13:26

Muhtasari


•Msemaji wa Jumba la ndondi la Hall of Famer alithibitisha kwamba Tyson alimpiga abiria mwenzake ambaye alimchokoza bila sababu.

Bondia wa zamani wa uzito wa juu Mike Tyson amempiga ngumi abiria mwenzake katika ndege baada ya mtu huyo "kumrushia chupa ya maji," msemaji wa Tyson amesema.

Video iliyochukuliwa kwenye ndege hiyo inamuonesha Tyson akiwa ameegemea kiti chake huku akimpiga ngumi za mara kwa mara mtu ambaye hakuonekana.

Msemaji wa Jumba la ndondi la Hall of Famer alithibitisha kwamba Tyson alimpiga abiria mwenzake ambaye alimchokoza bila sababu.

Polisi waliwaweka kizuizini watu wawili kwa muda.

Mtu mmoja alitibiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa San Francisco kwa kuwa alipata majeraha kidogo.

"Hawakutoa ushirikiano kwa polisi kufanya uchunguzi zaidi," msemaji wa Idara ya Polisi ya San Francisco alisema katika taarifa.

Wote wawili waliachiliwa huru "kusubiri uchunguzi zaidi". Idara ya polisi haikubainisha jina la mhusika yeyote.

Shambulio hilo lilitokea kwenye ndege ya JetBlue Jumatano usiku, kabla ya kuondoka San Francisco hadi Florida.

Video - iliyochapishwa na TMZ - haioneshi ugomvi wote na chupa ya maji kurushwa haioneshi.

Kwa mujibu wa TMZ, Tyson alikuwa amekubali kupiga picha na abiria mwanzoni mwa safari hiyo. Lakini mwanaume huyo aliendelea kumsumbua Tyson, licha ya Tyson kumuomba atulie.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved