logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usimuamini pasta wako muamini Mungu-Ushauri wa Huddah kwa Wakristo

Huddah anafahamika sana kwa semi zake mitandaoni, na pia kupitia bidii ya kazi yake.

image
na Radio Jambo

Habari24 April 2022 - 19:36

Muhtasari


  • Mwanasosholaiti maarufu nchini Huddah Monroe, ametoa ushauri wa kipekee kwa mashabiki wake ambao ni wakristo
Mwanasosholaiti Huddah Monroe

Mwanasosholaiti maarufu nchini Huddah Monroe, ametoa ushauri wa kipekee kwa mashabiki wake ambao ni wakristo.

Huddah anafahamika sana kwa semi zake mitandaoni, na pia kupitia bidii ya kazi yake.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram, katika Insta Stories Mwanasosholaiti huyo aliwashauri mashabiki wake wawee kumuamini Mungu wala sio muhubiri wao.

Ni nyakati nyingi ambazo wakristo wengi wamekuwa wakiwaamini wahubiri mbali mbali  na kuhudhuria kanisa kwa ajili ya kutendewa miujiza.

Wengi wao uamini kwamba hawana imani ya kujiombea na kupata walichoamini na kuombea.

Huddah alikuwa anajibu ujumbe unaosoma;

'Natamani wazazi wa Afrika wangesukuma masomo ya pesa jinsi wanavyosukuma dini."

Huddah alijibu na kusema;

"Dini imemaliza waafrika, amini Mungu na wala sio pasta wako," Alisema Huddah.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved