logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DRAMA!Jamaa asababisha drama bungeni huku akidai ni mjukuu wake Kibaki

Hata huku maafisa wa polisi wakijaribu kumfariji ili atulie, mwanamume huyo hangesikia lolote.

image
na Radio Jambo

Habari26 April 2022 - 08:12

Muhtasari


  • Hata huku maafisa wa polisi wakijaribu kumfariji ili atulie, mwanamume huyo hangesikia lolote

Mwanamume anayeomboleza amezua taharuki katika majengo ya Bunge jijini Nairobi ambapo mwili wa rais mstaafu Mwai Kibaki umelazwa.

Mtu huyo ambaye hakutambuliwa alidai kuwa yeye ni mjukuu wa mbali wa marehemu Mwai Kibaki, na alihuzunishwa sana na taarifa za kifo chake.

"Kwa nini umeenda haraka sana," alisema, huku akitokwa na machozi.

Hata huku maafisa wa polisi wakijaribu kumfariji ili atulie, mwanamume huyo hangesikia lolote.

“Niruhusu nimwone kwa mara ya mwisho,” aliwaambia maafisa hao.

Mwanaume huyo alitangulia kuvua baadhi ya nguo zake, akipinga aruhusiwe kuutazama mwili wa ‘babu yake’ aliyeanzisha elimu ya msingi bila malipo.

Baadaye maafisa wa polisi walimsindikiza mwanamume huyo kutoka kwa Majengo ya Bunge baada ya juhudi za kumtuliza kutozaa matunda.

Mwili wa rais mstaafu Mwai Kibaki uliwasili katika Majengo ya Bunge jijini Nairobi kutoka makafani ya Lee Jumanne asubuhi kwa siku ya pili ya kutazamwa na umma.

Wakenya ambao hawakuutazama mwili wa Mwai Kibaki siku ya Jumatatu sasa watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho.

Mwili wa Rais mstaafu Kibaki utaagwa kutoka Jumatatu hadi Jumatano.

Wakati huu, umma utaruhusiwa kuutazama mwili huo kabla ya Mazishi ya Kiserikali siku ya Ijumaa katika uwanja wa Nyayo.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved